Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Geita  Mhe. Zahara Michuzi ametembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa uwanja wa michezo unaojengwa eneo la Magogo mjini Geita (pichani chini) na kueleza kuwa mpaka kufikia mwezi wa 11 ujenzi huo  kwa awamu ya kwanza utakuwa umekamilika kwa asilimia 98% mpaka 100%.

Mhe Zahara amesema hilo linawezekana kwa sababu fedha ipo, mkandarasi yupo na vifaa vipo na vinafika saiti kwa wakati na kufikia tarehe 1 mpaka 15 ya mwez wa 11 uwanja huo utakuwa umekamilika kwa ajili ya matumizi.

"Matamanio yangu katika ujenzi wa uwanja (Geita Gold Stadium) ni kwamba mechi zote za Ligi Kuu na michuano mingine zinachezewa hapa ili wananchi wa Geita  waweze kupata burudani na shangwe hili la Ligi Kuu wakiwa nyumbani wakiangalia live"

"Sambamba na hilo naamini kupitia shangwe hilo la Ligi Kuu tutapata wageni wengi sana  ambao watatumia huduma mbali mbali ikiwemo hotel zetu watoa huduma za chakula pamoja na wenye vyombo vya usafiri, tunatamani kuona mzunguko wa fedha  unakuwa mkubwa na shughuli za  kimaendeleo zinakuwa zaidi."

"Kwa kweli niwahakikishie wana geita  wenzangu kwamba mkandarasi huyu wa sasa hivi kwanza anavifaa vya kutosha na pia kutokana na ukaguzi wetu wa mara kwa mara  na wahandisi wetu muda mwingi tuko saiti kuhakikisha wanatimiza majukumu yao kutokana na mipango mikakati ya kazi zao." ameeleza Mhe. Zahara.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...