Na Mwandishi wetu, Hanang’

 

MBUNGE wa viti maalum wa Vijana Taifa kupitia Mkoa wa Manyara, Asia Halamga, amekamilisha mbao za upauzi wa nyumba mpya ya Katibu wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana UVCCM Wilaya ya Hanang’ baada ya kukabidhi mbao 214.

 

Asia amekabidhi mbao hizo baada ya kuzindua rasmi jana Hanang’ Vijana Jogging Club ambapo alikuwa mgeni rasmi wa mazoezi hayo yaliyoanzia ofisi za ofisi za CCM Wilaya mji mdogo wa Katesh na kuishia uwanja wa shule ya msingi Katesh.

 

Akizungumza wakati akikabidhi mbao hizo Asia amesema katika hatua ya upauaji zilikuwa zinahitajika mbao 214 na akaonelea azunguke kwa wadau mbalimbali wa maendeleo ili kukamilisha lengo la upauzi wa nyumba hiyo.

Amesema alikutana na mdau wa maendeleo wa mjini Babati, Emmanuel Khambay ambaye alijitolea mbao 104 za kupaulia na yeye akamalizia hizo 110 za kukamilisha upauaji.

 “Hapa ni nyumbani na kila ninapokuwa nakuja sipendi kuja patupu nakuja na jambo fulani na jambo hilo ndiyo hili la kukamilisha mbao za ujenzi wa nyumba ya mtumishi wa UVCCM Hanang’,” amesema Asia.

 Amesema ili nyumba hiyo ikamilike inapaswa kupauliwa kwa mabati na mifuko kadhaa ya saruji hivyo wadau wengine wa maendeleo hasa vijana wanapaswa kushiriki kuikamilisha.

 Mwenyekiti wa UVCCM Wilayani Hanang’ Yohane Leonce amemshukuru Asia kwa moyo wa kujitolea kwa kuwaunga mkono katika kufanikisha maendeleo hasa ujenzi wa nyumba hiyo.  

 “Kwa niaba ya vijana wa Hanang’ tunakushukuru na kukupongeza kwa kujitolea kutuunga mkono katika ujenzi wa nyumba ya katibu wetu wa UVCCM Hanang’,” amesema Leonce.


Mdau wa maendeleo wa mjini Babati, Emmanuel Khambay amesema akiwa mzaliwa wa mkoa wa Manyara, anajivunia kuwaunga mkono vijana hao kwa kutoa mbao hizo 104.

Khambay amesema wataendelea kuungana mkono katika kufanikisha maendeleo kwani Manyara itajengwa na wana Manyara wenyewe na siyo vinginevyo.

 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...