Mtanange wa utangulizi wa ufunguzi Tamasha la Kizimkazi 2021 kati ya wenyeji Kizimkazi Mkunguni FC dhidi ya Mtende FC ilipigwa jana jioni katika dimba la Mgombewa, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, ambapo wenyeji hao walitamba nyumbani kwa kuwachabanga mabao 3-0 wana Mtende FC. Mchezo huo na mingine mingi itakayoendelea ni sehemu ya michuano kuelekea maadhimisho ya siku ya Tamasha la Kizimkazi hapo Agosti 28, 2021 lililo dhaminiwa na Benki ya CRDB na kufanyika Mkoa wa Unguja Kusini, Zanzibar. Mchezo huo ulikuwa ni wa kuvutia na wenye hisia kali kwa kila upande, vibweka pia havikukosekana.
Beki wa Timu ya Kizimkazi Mkunguni FC akiwa ameruka juu kumdhibiti Mshambuliaji wa timu ya Mtende FC wakati mtanange huo uliopiga jana jioni katika dimba la Mgombewa, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar
Vumbi lilitimka kweli kweliiii....
Vyenga kama vyote, jamani kuna vipaji hukuuuu..... Wale Aseno kama vipi waje tu huku kujichagulia.... (Utani kidogo)
haya tupishane.

Mimi na wewe ni Damu Damu (alisikika mshambuliaji huyu).
Mpira wenyewe ukwapi sasa??
Beki wa Mtende akiokoa goli.
Daktari wa Timu akienda kutoa huduma ya kwanza kwa mchezaji wake.
 Kala zote.







                          Wajasiriamali nao hawakua mbali........




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...