Mlundikano wa wanafunzi wa  shule za  Msingi na Sekondari madarasani umeonekana kurudisha nyuma kampeni ya kudhibiti  maambukizi ya ugonjwa wa UVIKO 19  mashuleni hivyo kuhatarisha  afya za wanafunzi hao.

Uchunguzi uliofanywa na Blog hii umebaini kuwa baadhi ya shule hazichukui tahadhari za kuwalinda wanafunzi na mambukizi ya UVIKO licha ya serikali kusisitiza mara kwa mara wananchi kuchukua tahadhari.

 Dk.Jairy Khanga ni mganga mkuu wa hospitali ya mkoa wa Ruvuma ambapo amewataka maafisa elimu pamoja na  ,walimu Mkoani humo kuendelea kufata muongozo wa udhibiti wa maambukizi wa UVIKO 19 katika shule za  Msingi na sekondari ,vyuo na taasisi za elimu uliotolewa julai mwaka huu na kuwasimamia  wanafunzi ili waweze kuchukua tahadhari ya maambukizi hayo hasa wakiwa mashuleni.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii,Dk.Khanga alisema,jukumu la kutoa elimu i la wadau wote  na tayari  wataalam wa afya  walitoa  mafunzo kwa maafisa elimu ambao wanapaswa  kuwasimamia wanafunzi  mashuleni  wakati wote  ili kuwakinga na maambukizi hivyo walimu na walezi  wanapaswa kuendelea kuwasaidia wanafunzi kuchukua tahadhari  .

Kwa Upande wake Mwanafunzi shule ya Msingi Ally Juma  alisema mlundikano Darasani ni mkubwa hakuna nafasi ya mita moja pia hata wasiponawa mikono au kutovaa barakoa walimu hawawaulizi hivyo wanaona kama hakuna ugonjwa wa UVIKO19.

"Hatunawi mikono ,waa hatuvai barakoa tulivaa tulipofungua tu shule lakini sasa hivi tunaendelea kusoma bila mashariti mimi naona kama ugonjwa umeisha , kwani zamani wazazi walituzuia kwenda shule na kushika vitu na kila muda walimu na hata wazazi majumbani walisema tunawe mikono na kutuzuia kucheza kwenye mikusanyiko"alisema Mariam

kwa upande wake Mwanafunzi  Faraja Batazar  mwanafunzi ruhila shule ya Msingi aisema mlundikano madarasani ni mkubwa na wanafunzi hawavai barakoa bali wanaendelea na masomo yao ya kila siku ambapo amekuwa akijifunika kitambaa pindi akikumbuka kuwa kuna ugonjwa huo.

"wanafunzi wacheza ,wanashikana mikono bila kunawa hivyo tunaweza kuambukizwa  UVIKO 19  , tunaomba walimu watusaidie"alisema

Kwa upande wake Ofisa elimu Mkoa wa Ruvuma Emmanuel Kisongo amekiri kuwepo kwa mlundikano mkubwa wa wanafunzi na kuwa baadhi ya shule zimekuwa hazichukui tahadhari ambapo amewataka kuendelea kuchukua tahadhari ya kujilinda na UVIKO 19 

Aliongeza kuwa Jukumu la kutoa elimu mashuleni ni la Wizara ya ya afya ila wataendelea kuwaelimisha watoto kujilinda na ugonjwa huo kipindi chote wanapokuwa shuleni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...