Na Mwamvua Mwinyi,Kibiti
Wanawake
 wa eneo la Bungu ,Wilayani Kibiti wanatarajia kuondokana na  changamoto
 kubwa ya ufinyu wa chumba cha kujifungulia waliyoipata kwa zaidi ya 
miaka 25 iliyopita baada ya kukamilika kwa jengo la wodi ya wazazi na 
choo zahanati ya Bungu.
Wanawake
 hao kipindi hicho walitaabika kuzaa kwa mbanano na wengine kuzalia 
chini ,kutokana na ufinyu wa chumba na upungufu wa vitanda ambapo 
vilikuwa vitanda viwili .
Pamoja
 na hayo ,kulikuwa na kero ya maji iliyosababisha mjamzito kwenda 
kujifungua na maji kutoka nyumbani na vibatari kwa kukosekana nishati ya
 umeme.
Akizindua jengo 
la wodi ya wazazi na choo katika zahanati ya Bungu , kiongozi wa mbio 
maalum za mwenge wa uhuru ,LT.Josephine Mwambashi alisema , serikali 
inajitahidi kuhakikisha inaondoa matatizo ya upungufu wa majengo ya 
uzazi na upasuaji.
Alisema , serikali pia inapambana kutatua changamoto mbalimbali za afya ikiwemo vifaa tiba ,dawa na majengo mbalimbali.
Akitoa
 taarifa ya mradi mganga mfawidhi zahanati ya Bungu,Luhalala Jackson 
alielezea,umegharimu milioni 40 ,387,457 zikiwa ni fedha kupitia mradi 
wa malipo kwa ufanisi (RBF).
"Mradi
 huu una faida kubwa kwa wananchi wa Bungu na maeneo jirani hususan 
akinamama wajawazito wanaofika kituoni kwa ajili ya huduma za uzazi "
Luhalala
 alifafanua ,lengo ni kupunguza vifo vya akinamama wajawazito na watoto 
wachanga kwa kuhakikisha wanapata huduma bora na kwa wakati .
Alibainisha
 ,wastani zahanati hiyo inahudumia wagonjwa 16,292 (OPD) ambapo wanaume 
ni 7,210 na wanawake 9,082 kwa mwaka ,kwa wiki wanajifungua kina mama 15
 sawa na wateja 60 kwa mwezi ,ambapo kwa mwaka mzima ni wateja 400 hadi 
720.
Mkazi wa Bungu 
,Amina Mnjopeka alisema ,wanaishukuru serikali kwa kusogezewa huduma 
hiyo kwani miaka zaidi ya 20 walitaabika hasa katika tatizo la chumba 
kidogo cha kuzalia,maji na umeme.
Mwenge wa uhuru umepokelewa Kibiti agost 15 ukitokea Rufiji na agost 16 Jumatatu utapokelewa Wilayani Mkuranga.




Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...