Na Amiri Kilagalila,Njombe

Ikiwa ni siku chache tangu waziri wa Nchi ofisi ya Rais tawala za mikoa na serikali za mitaa Ummy Mwalimu kuagiza kuanza mara moja ujenzi wa ofisi za halmashauri ya wilaya ya Njombe.Timu ya wataalamu kutoka halmashauri hiyo iliyoambatana na mkurugenzi imetembelea na kukagua maeneo makubwa matatu ya halmashauri iliyokabidhiwa na wananchi wa kijiji cha Kidegembye bure ili kuanza ujenzi.

Akitoa taarifa ya vipimo ya eneo mojawapo mara baada ya timu hiyo kukagua,Afisa wa mipango miji wilaya ya Njombe Erick Chigome amesema eneo mojawapo mara baada ya kufanyiwa vipimo limebainika kuwa na ukubwa wa ekari 75 na kuwa na utosherevu wa ujenzi wa taasisi za serikali takribani 20

“Kwa ujumla tulivyofika na kulipima eneo hili limetoa ekari 75 na kwasababu hiyo tunakusudia kuwa na taasisi takribani 20 na wananchi wameridhia eneo hili na kutoa eneo hili kwa ajili ya ujenzi wa halmashauri”alieleza Chigome

Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo Valentino Hongoli amewashukuru wananchi kwa kutoa eneo hilo kubwa bila ya kuwa na fidia yeyote na kuwaagiza wataalamu kuja na ushauri mzuri juu ya ujenzi katika maeneo hayo likiwemo eneo lingine la ekari 10 la karibu ndani ya kijiji hicho ambalo tayari lilishapatikana BOQ.

“Haya ni maeneo yetu lakini wataalamu mtushauri ipasavyo na waziri alishatupa ushauri,na kama ninyi wataalamu mnaona kwamba hakuta kuwa na mtikisiko wowote wa bajeti basi tunaweza tukaja hapa kwenye ekari 75 badala ya pale kwenye ekari 20.Mfano pale tumetumia milioni 48 za kupimia tu kwa hiyo tunawategemea wataaalamu kuona tunafanyaje”alisema Hongoli

Aidha amesema kwa kuwa eneo la karibu lenye ekari 10 tayari limeshapimwa na BOQ imepatikana wanategemea kuanza moja kwa moja ili kupunguza muda wa ujenzi na hatua za upimaji katika eneo hilo jingine lenye ekari 75.

“Pale kwenye ekari 10 pameshapimwa tayari kilichobakia ni utekelezaji tu tungeenda haraka lakini pia bara bara ya Lami inapita kule kwa hiyo tukijenga hapa mwananchi atalazimika pia kuongeza ghalama,sisemi hivi ili kubatilisha mawazo ya wataalamu kama mna ona hatutaathiri bajeti wala hatutachelewa tunawasikiliza ninyi”aliongeza Hongoli

Kwa upande wake mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Njombe Bi,Sharifa Yusuph Nabarang’anya  amesema wanatamani kuona taasisi zinapatikana katika eneo moja ili kuwasaidia wananchi kupata huduma kwa haraka huku akishukuru wananchi wa kijiji hicho kwa kutoa eneo tayari kwa kuanza ujenzi.

“Tumelipokea eneo hili na tuko tayari kuanza taratibu nyingine za ujenzi na kabla ya ujenzi tutatoa taarifa katika maeneo haya mawili ni wapi tutaenda kujenga”alisema Bi,Sharifa Yusuph Nabarang’anya  

Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya hiyo Bi,Sharifa Yusuph Nabarang’anya  aliyeongozana na wataalamu ametembelea na kuyapokea maeneo yote matatu moja lenye ekari 75 na lenye ekari 10 huku moja likiwa bado halijabainika ukubwa wake na maeneo yote yakiwa yanapatikana katika kitongoji cha Ikombe kijiji cha Kidegembye.
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Njombe Bi,Sharifa Yusuph Nabarang’anya  akizungumza mara baada ya kukagua na kupokea eneo la ujenzi wa ofisi za halmashauri na kuahidi kuanza ujenzi mara moja.
Baadhi ya wataalamu wakimuonyesha mkurugenzi mwisho wa eneo la halmashauri hiyo walilokabidhiwa na wananchi kwa ajili ya ujenzi wa ofisi za halmashauri.

Viongozi wa kijiji cha Kidegembye na timu ya wataalamu wakizunguka na kukagua eneo la ujenzi wa ofisi lenye ukubwa wa ekari 75
Diwani wa kata ya Kidegembye akimuonyesha mkurugenzi mwisho wa eneo jingine ambalo bado halijawekwa wazi vipimo vyake walilotoa wananchi kwa ajili ya matumizi ya halmashauri.
Picha ya eneo la ekari 75 ambalo limependekezwa na waziri wa TAMISEMI kuwa ingefaa eneo hilo kujengwa ofisi za halmashauri.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...