Mkururgenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni Melkzedeki Humbe na Aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya hiyo  Charles Fussi (ushoto) wakikabidhiana ofisi.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni Jumanne Mlagaza (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wakurugenzi hao.

Wakurugenzi Melkzedeck Humbe (kushoto) na Charles Fussi wakiwa katika picha ya pamoja baada ya makabidhiano ya ofisi.

Mkurugenzi Charles Fussi (wa pili kulia) na Afisa Kilimo Fadhili Chimsala na Mkaguzi wa Ndani, Rweikiza wakimuonesha mashamba ya korosho Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Halmashauri ya Wilaya ya  Manyoni, Melkzedeck Humbe.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni, Jumanne Mlagaza akitoa shukrani kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni, Charles Fussi kwa kuweza kukabidhi ofisi kwa mkurugenzi aliyechukua nafasi yake.

Wakuu wa Idara na vitengo wakiwa katika picha ya pamoja na Wakurugenzi na Mwenyekiti wa Halmashauri baada ya sherehe hiyo ya makabidhiano.


Na  Alinikyisa Humbo, Manyoni 


ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni  Charles Fussi amemkabidhi ofisi Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Halmashauri hiyo Melkzedeck Humbe katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika jana wilayani humo.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa ofisi Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Halmashauri hiyo Melkzedeck Humbe alisema anategemea ushirikiano mkubwa kutoka kwa viongozi wa Halmashauri hiyo, wakuu wa idara na watumishi wote.

Humbe alisema kwamba bila ushirikiano hakuna kitakachoweza kufanyika ambapo alitumia nafasi hiyo kumpongeza  aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Charles Fussi kwa kazi kubwa aliyoifanya kwa kipindi chote alichoweza kuhudumu hasa katika usimamimizi wa shughuli zote za maendeleo na ubunifu wa mradi wa kilimo cha korosho.

"Sijaja hapa kuanzisha kazi bali nimekuja kuendeleza kazi iliyoachwa na mtangulizi wangu Fussi na kwamba kama ambavyo kauli ya Rais Samia Suluhu isemavyo kwamba kazi iendelee basi ndivyo ninavyotamani Manyoni iendelee kazi alizokuwa akiifanya mwenzangu ziendelee". alisema Humbe.

Alisema amefika Manyoni kuendeleza yale yote ambayo Fussi aliweza kuyaibua ikiwa ni utekelezaji wa ilani na si vinginevyo.

Kwa upande wake Fussi amewashukuru watumishi wote na kuahidi kwamba ataendelea kutoa ushirikiano pale watakapoona inafaa ili kuleta tija ya maendeleo kwa wananchi wa Wilaya ya Manyoni.

Aidha Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni, Jumanne Mlagaza alitoa shukrani kwa Fussi kwa kipindi chote walichoweza kufanya kazi pamoja na kuwa anaamini Mkurugenzi aliyekabidhiwa ofisi ataendeleza ushirikiano wa utendaji kazi kati ya Ofisi ya Mkurugenzi na ofisi yake.

Makabidhiano hayo yamehudhuriwa na Wakuu wa Idara na Vitengo vyoe na,Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni na baada ya makabidhiano ya ofisini ya nyaraka basi waliweza pia kutembelea mradi mama wa kilimo cha korosho katika maeneo yote yalipo mashamba hayo wilayani humo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...