NA TIGANYA VINCENT
MKUU wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt.Batilda Buriani ameagiza kufungwa kwa Mfumo wa wa utoaji wa taarifa katika vituo vya Serikali vya kutolea huduma za afya GOTHMIS ili kudhibiti upotevu wa mapato.
Alisema kukosekana kwa Mifumo huo katika baadhi ya maeneo ya utoaji wa huduma za afya za Seikali kumesababisha upotevu wa fedha za umma nakuishia mifukoni mwa watu wachache.
Balozi Dkt. Batilda ametoa kauli hiyo leo mjini Tabora baada ya kukutana na Wajumbe wa Baraza la Watu wanaishi na VVU Tanzania na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu -Sera, Uratibu na Bunge Kaspar Mmuya
Alisema katika Zahanati ambazo zimeanza kutumia mfumo GOTHIMS mapato yao yamepanda mara mbili.
“Kuna Kituo cha Afya wilayani Urambo waliokuwa wakipata kiasi cha shilingi laki tatu kwa mwezi lakini baada ya kufunga mfumo wa GOTHIMS mwezi wa kwanza mapato yalipanda na kufikia milioni saba na Mwezi uliofuata walipata milioni 10…hii inaonyesha kuwa fedha nyingi zilikuwa zikiishia mifukoni mwa watumishi wasio waaminifu”alisema
Aidha Mkuu huyo wa Mkoa wa Tabora amewaonya Wahasibu kutoharibu mifumo kwa ajili ya kutaka wakusanye mapato kwa mfumo wa zamani.
Alisema ikibainika watachukuliwa hatua ikiwemo kufikishwa katika vyombo vya Sheria.
MKUU wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt.Batilda Buriani ameagiza kufungwa kwa Mfumo wa wa utoaji wa taarifa katika vituo vya Serikali vya kutolea huduma za afya GOTHMIS ili kudhibiti upotevu wa mapato.
Alisema kukosekana kwa Mifumo huo katika baadhi ya maeneo ya utoaji wa huduma za afya za Seikali kumesababisha upotevu wa fedha za umma nakuishia mifukoni mwa watu wachache.
Balozi Dkt. Batilda ametoa kauli hiyo leo mjini Tabora baada ya kukutana na Wajumbe wa Baraza la Watu wanaishi na VVU Tanzania na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu -Sera, Uratibu na Bunge Kaspar Mmuya
Alisema katika Zahanati ambazo zimeanza kutumia mfumo GOTHIMS mapato yao yamepanda mara mbili.
“Kuna Kituo cha Afya wilayani Urambo waliokuwa wakipata kiasi cha shilingi laki tatu kwa mwezi lakini baada ya kufunga mfumo wa GOTHIMS mwezi wa kwanza mapato yalipanda na kufikia milioni saba na Mwezi uliofuata walipata milioni 10…hii inaonyesha kuwa fedha nyingi zilikuwa zikiishia mifukoni mwa watumishi wasio waaminifu”alisema
Aidha Mkuu huyo wa Mkoa wa Tabora amewaonya Wahasibu kutoharibu mifumo kwa ajili ya kutaka wakusanye mapato kwa mfumo wa zamani.
Alisema ikibainika watachukuliwa hatua ikiwemo kufikishwa katika vyombo vya Sheria.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...