Na Amiri Kilagalila,Njombe
Viongozi
wa dini nchini wameshauriwa kuacha kuwapotosha wananchi kuhusu chanjo
ya Corona kwani kufanya hivyo ni kuiingilia serikali katika kutimiza
majukumu yake kwa wananchi inaowasimamia.
Kauli
hiyo imetolewa na Mwinjilisti Asifiwe Mwasanyamba wa Kanisa la Kiinjili
na Kirutheli Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kusini usharika wa Melinze
mkoani Njombe wakati wa ibada ya kuliombea taifa kwa siku nane ili
kuondokana na ugonjwa wa Uviko 19.
“Kuna
wengine wanapotosha kwa kusema chanjo hii ni mbaya,niwaulize ni nani
aliyechoma hapa Tanzania akaona ni mbaya? Niseme tu serikali imewajibika
na ingekuwa ya ajabu kama isingeonyesha kuwajibika na niwaaambie wakati
wa vita hatuchagui silaha kwa hiyo lazima silaha yoyote
tuitumie”Alisema Asifiwe Mwasanyamba
Mwasanyamba
ameongeza kuwa “Tusisikilize propaganda kwasababu wasemaji wa serikali
tunao,hawa wakisema juu ya taifa tuwasikilize na kwa kuwa kuna wengine
wanapotosha juu Chanjo hawa tuwapuuze.Kwa hiyo sisi kama wainjilisti
tunasema hivi mtu akitaka Chanjo achanjwe na asipotaka asichanjwe”
Kwa
upande wake kiongozi wa usharika huo mchungaji Eliad Siwelwe amesema
kanisa hilo limekuwa likiwatahadharisha waumini wake kunawa mikono na
kuvaa barakoa wanapokuwa kwenye ibada na hata wakiwa kwenye shughuli
zingine ili kuendelea kupambana na virusi vya Corona.
“Juu
ya chanjo tunawahimiza watu waweze kuchanja kwasababu kila mtu na imani
yake lakini pia tumekuwa tukiwahamasisha waumini kuendelea kuchukua
tahadhari kwa kufuata njia zote za kujikinga na corona” Eliad Siwelwe
Mchungaji kiongozi Usharika wa Melinze
Baadhi
ya waumini wa kanisa hilo akiwemo Amina Ilomo na Osward Mng'ong'o
wanasema tahadhari dhidi ya Uviko 19 wanachukua ingawa mpaka sasa baadhi
yao hawajaamua juu ya kupokea chanjo ya Uviko 19 na kuendelea
kusisitizana kila mmoja afaute nafsi yake,
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...