Na Amiri Kilagalila
Kutokana
na ufanisi wa mbegu ya asili iliyoonyeshwa na shirika la MVIWATA, afisa
tarafa ya Mchauru wilayani Masasi Titho Stambuli ameagiza maafisa
watendaji kutoa ushirikiano kwa shirika Hilo.
Stambuli
ametoa agizo hilo alipokuwa mgeni rasmi kwenye maonyesho ya mbegu za
Asili yaliyoandaliwa na shirika hilo yaliyofanyika kiwilaya katika kata
ya Mchauru kijiji cha Namombwe,
"Shirika
la MVIWATA ni nguzo mhimu katika kuwainua wakulima,kuwajengea uwezo,
uhifadhi wa mbegu,kuongezeka kwa uzalisha na ni watetezi wa
wakulima"Alisema Stambuli
Aidha amesema ofisi yako ipo tayari kutoa ushirikiano wa hali na mali kwa shirika hilo ili kuwaletea maendeleo wakulima.
"Nimeagiza
watendaji kutoa ushirikiano kwa shirika na pia kwangu milango iko wazi
katika kuwapa ushirikiano ili mradi mkulima anufaike na shirika"
Vile
vile bwana Stambuli amesema serikali inaendelea kutatua kila aina ya
Changamoto inayo mkuta mkulima ikiwemo swala la pembejeo ili kufanya
kilimo chenye tija na shirika la Mviwata kuwa na tija kwa jamii kwa
kupata matokeo chanya
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...