Na Amiri Kilagalila

Kutokana na ufanisi wa mbegu ya asili iliyoonyeshwa na shirika la MVIWATA, afisa tarafa ya Mchauru wilayani Masasi Titho Stambuli ameagiza maafisa watendaji kutoa ushirikiano kwa shirika Hilo.

Stambuli ametoa agizo hilo alipokuwa mgeni rasmi kwenye maonyesho ya mbegu za Asili yaliyoandaliwa na shirika hilo yaliyofanyika kiwilaya katika kata ya Mchauru kijiji cha Namombwe,

"Shirika la MVIWATA ni nguzo mhimu katika kuwainua wakulima,kuwajengea uwezo, uhifadhi wa mbegu,kuongezeka kwa uzalisha na ni watetezi wa wakulima"Alisema Stambuli

Aidha amesema ofisi yako ipo tayari kutoa ushirikiano wa hali na mali kwa shirika hilo ili kuwaletea maendeleo wakulima.

"Nimeagiza watendaji kutoa ushirikiano kwa shirika na pia kwangu milango iko wazi katika kuwapa ushirikiano ili mradi mkulima anufaike na shirika"

Vile vile bwana Stambuli amesema serikali inaendelea kutatua kila aina ya Changamoto inayo mkuta mkulima ikiwemo swala la pembejeo  ili kufanya kilimo chenye tija na shirika la Mviwata kuwa na tija kwa jamii kwa kupata matokeo chanya

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...