Waziri
wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Innocent Bashungwa,
amewataka BAKITA kutumia tehama ili kuweza kukuza wigo wa lugha ya
Kiswahili katika mataifa mbalimbali duniani ili kuwapa fursa watalaam wa
Kiswahili waliopo nchini
“Bakita tumieni njia
za kielekroniki sasahivi ulimwengu umehama upo mtandaoni, idara ya
Tehama kazeni tumieni mitandao ya kijamii kutangaza fursa za lugha la
Kiswahili ili mtu wa nchi za nje akitaka kujifunza kupitia machapisho
yenu ajifunze na hii itatoa fursa kwa wataalam wetu kwani kiswahili kwa
sasa kina mahitaji makubwa duniani”, Waziri Bashungwa.
Waziri
Bashungwa ametoa maagizo hayo leo Agosti 2, 2021 Jijini Dar es Salaam
alipofanya ziara katika ofisi za Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA)
na kuwaagiza kuanza kutumia njia mpya yakujitangaza na kutangaza
kiswahili nchini na kuachana na mifumo ya kizamani
Pia
Waziri Bashungwa aliwataka BAKITA kuangalia fursa za kuanzisha vituo
vya mafunzo ya kiswahili katika Balozi mbalimbali Duniani ili
Kuunganisha Kiswahili na utalii utakaokuza lugha hiyo ambayo ni ya kumi
kati ya lugha zinazozungumzwa sana Duniani pamoja na Utamaduni wa
Tanzania.
Katika ziara hii Mhe. Bashungwa
alitembelea darasa la kisasa la kufundishia wakalimani lililofungwa
vifaa vya kisasa ambalo bado halijafunguliwa rasmi kwa sasa.
Kwa
upande wake Kaimu Mtendaji Mkuu wa BAKITA, Bi. Consolata Mushi
amemueleza Mhe. Waziri kuwa baraza hilo limejipango mwaka wa fedha wa
2021/2022 kuongeza idadi ya wakalimani kufikia 50 nchini ili kukidhi
hitaji la ukalimani ili kukidhi tija ya huduma hii nchini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...