Waziri wa Kilimo Mhe. Prof. Adolf Mkenda (Mb) akiwa ameambatana na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe Antony Mtaka wakimkabidhi zawadi ya Televisheni Afisa Ugani Kata ya Ng'humbi Ndg Charles Mujule kama kielelezo cha kufanya kazi kwa ufanisi wakati alipokutana na kuzungumza na maafisa ugani wa Wilaya ya Kongwa katika Mkoa wa Dodoma, kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Kongwa, tarehe 17 Agosti 2021.

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Kongwa

Waziri wa Kilimo Mhe. Prof. Adolf Mkenda (Mb) jana tarehe 17 Agosti 2021 amemkabidhi zawadi ya Televisheni Afisa Ugani Kata ya Ng'humbi Ndg Charles Mujule kama kielelezo cha kutambua utekelezaji wa kazi yake.

Waziri Mkenda ametoa zawadi hiyo wakati wa kikao kazi alipokutana na kuzungumza na maafisa ugani wa Wilaya ya Kongwa katika Mkoa wa Dodoma, kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Kongwa.

Amesema kuwa maafisa ugani ndio mboni ya jicho la Wizara ya Kilimo hivyo ili nchi iweze kuwa na kilimo bora kinachokidhi matakwa ya tija na wingi wa uzalishaji na kuwa na kilimo kitakachokidhi matakwa ya soko ni wazi kuwa elimu ni muhimu itolewe kwa wakulima.

Waziri wa Kilimo amesisitiza kuwa bila kufanya kazi kwa ufanisi na maafisa ugani kilimo hakiwezi kupiga hatua za kimaendeleo hivyo serikali imekuja na mkakati wa kuwatambua na kuwapa mashamba ili wawe mfano kwenye sekta ya kilimo.

Akizungumza katika mkutano huo mara baada ya kukabidhiwa zawadi hiyo awfisa Ugani wa Kata ya Ng'humbi Ndg Charles Mujule amemshukuru Waziri Mkenda kwa kutambua na kuthamini kazi kubwa zinazofanywa na maafisa ugani nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...