Na Mwamvua Mwinyi,Kibiti


MKUU wa Mkoa wa Pwani ,Abubakar Kunenge amemuagiza mkandarasi anayejenga  daraja la Mbuchi ,wilaya ya Kibiti kuharakisha ujenzi ili  kuwaondolea kero wananchi wanayoipata kwa sasa.

Kunenge aliyasema hayo ,alipokuwa kwenye ziara ya Kamati ya siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoa huo ilipokuwa ikikagua miradi ya maendeleo likiwemo daraja hilo la Mbuchi

Kunenge alisema kukamilika kwa daraja hilo kutafungua njia kwa wakazi wa Vijiji vya Mbwela ambao wanasafirisha bidhaa kwenda Muhoro na maeneo mengine ya Wilaya ga Rufiji.

Mkuu huyo wa Mkoa alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha za miradi ya maendeleo ambayo inaondoa kero kwa wananchi.

Kaimu Mhandisi Mkazi wa Mradi huo Mtani Silasi alisema mradi huo utatekelezwa kwa miezi 12 na kwamba hadi kukamilika utagharimu kiasi cha shilingi Bilion 6.1.










Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...