Na Amiri Kilagalila,Njombe
Jeshi
la polisi mkoani Njombe linamshikilia mwanamke aliyefahamika kwa jina
la Vaileth Chaula (30) mkazi wa kijiji cha Mkongomi kata ya Kidugala
wilayani Wanging'ombe kwa tuhuma za kumuua mtoto wake wa kumzaa Azgad
(3) kwa kumkata na shoka kichwani na kupelekea kifo chake.
Kamanda
wa polisi mkoa wa Njombe Hamisi Issah amesema kwa mujibu wa maelezo ya
wanandugu mwanamke huyo alikuwa na matatizo ya akili.
Alisema
miezi michache iliyopita mwanamke huyo akiwa Makambako alipokuwa
ameolewa alipatwa na matatizo ya akili na kurudishwa nyumbani kwao kwa
wazazi wake ili apatiwe matibabu.
Alisema
akiwa na mtoto huyo ambaye alionekana kudeka, mama yake huyo aliona kuwa
anasumbuliwa na mtoto huyo hivyo alichukua shoka ili kumkata kata mtoto
huyo.
"Huo ni ukatili tunaita ingawa huyu mama ni mgonjwa lakini sasa sheria haisemi namna hiyo" alisema Issah.
Alisema
mwanamke huyo anashikiliwa na jeshi hilo likiwa linasubiri kukamilika
kwa baadhi ya mambo ili aweze kufikishwa mahakamani.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...