Na Amiri Kilagalila,Njombe

Jeshi la polisi mkoani Njombe linamshikilia mwanamke aliyefahamika kwa jina la Vaileth Chaula (30) mkazi wa kijiji cha Mkongomi kata ya Kidugala wilayani Wanging'ombe kwa tuhuma za kumuua mtoto wake wa kumzaa Azgad (3) kwa kumkata na shoka kichwani na kupelekea kifo chake.

Kamanda wa polisi mkoa wa Njombe Hamisi Issah amesema kwa mujibu wa maelezo ya wanandugu mwanamke huyo alikuwa na matatizo ya akili.

Alisema miezi michache iliyopita mwanamke huyo akiwa Makambako alipokuwa ameolewa  alipatwa na matatizo ya akili na kurudishwa nyumbani kwao kwa wazazi wake ili apatiwe matibabu.

Alisema akiwa na mtoto huyo ambaye alionekana kudeka, mama yake huyo aliona kuwa anasumbuliwa na mtoto huyo hivyo alichukua shoka ili kumkata kata mtoto huyo.

"Huo ni ukatili tunaita ingawa huyu mama ni mgonjwa lakini sasa sheria haisemi namna hiyo" alisema Issah.

Alisema mwanamke huyo anashikiliwa na jeshi hilo likiwa linasubiri kukamilika kwa baadhi ya mambo ili aweze kufikishwa mahakamani.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...