Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro amesema kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Nchini Rwanda wameazimia kwa moja kukabiliana na makosa yanayovuka mipaka ikiwemo makosa ya ugaidi kutokana na mkakati waliojiwekea mwezi Mei mwaka huu jijini Dar es salaam.
IGP Sirro amesema hayo jana muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa J. K. Nyerere jijini Dar es salaam wakati akitokea nchini Rwanda kwa ziara ya kikazi ya siku tatu iliyolenga kuboresha ushirikiano wa matukio mbalimbali ya uhalifu na wahalifu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...