Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzanzania, Samia Suluhu Hassan atakuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa Tamasha la Michezo kwa wanawake litakalofanyika katika viwanja vya Uhuru na Mkapa kuanzia siku ya kesho Septemba 16  jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa Habari, Katibu Mkuu wa Wizara ya Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Hassan Abbas amesema kauwa Mh. Rais atazindua tamasha hilo la siku tatu ambalo litashirikisha Michezo mbalimbali kwa wanawake.

“Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  anatarajia kuzindua tamasha la kwanza la Michezo la Tanzanite siku ya Jumamosi lenye lengo la kuitangaza nchi kupitia sekta ya Michezo ambalo Michezo na burudani mbalimbali zitakuwepo,” amesema Dkt. Abbas.

Dkt. Abbas amesema kuwa tamasha hilo litaanza kwa kutoa mada mbalimbali siku ya kesho zenye lengo la kuongeza uelewa wa umuhimu wa ushiriki wa Michezo kwa wanawake na kufuatiwa na Michezo tofauti katika viwanja vya Uhuru na Mkapa.

“Mheshimiwa Rais akiwa jijini Mwanza akizungumza na vijana alisisitiza sana juu ya sekta ya Michezo hapa nchini na kurudisha Michezo mashuleni na tunategemea kupitia tamasha hili tunatarajia kupata vijana wengi wenye vipaji,” amesema Dkt. Abbass.

Aidha Dkt. Abbass ameongeza kuwa tamasha hilo la siku tatu litakuwa ni la bure na hivyo kuwahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi kujionea burudani mbalimbali za Michezo zitakazotolewa na wanawake.

Katibu Mkuu Wizara ya Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Hassan Abbas (katikati) akifafanua jambo kwa waandishi wa Habari (hawapo pichani) wakati akizungumza nao mapema hii leo jijini Dar es Salaam Septemba 15 juu ya Tamasha la Michezo kwa wanawake litakalofanyika katika viwanja vya Uhuru na Mkapa kuanzia siku ya kesho Septemba 16  jijini Dar es Salaam, kushoto ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo wa wizara hiyo, Yusuph Singo na kulia ni Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo (BMT) Bi. Neema Msitha.
Waandishi wa Habari wakimsikiliza Katibu Mkuu Wizara ya Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Hassan Abbas (katikati) wakati akizungumza nao mapema hii leo jijini Dar es Salaam Septemba 15 juu ya Tamasha la Michezo kwa wanawake litakalofanyika katika viwanja vya Uhuru na Mkapa kuanzia siku ya kesho Septemba 16  jijini Dar es Salaam, kushoto ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo wa wizara hiyo, Yusuph Singo na kulia ni Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo (BMT) Bi. Neema Msitha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...