Mshauri wa Chama cha Skauti wa Kike cha Tanzania Girl Guides (TGGA),Victoria Mushi akiwafundisha kuyajua malengo yanayokusudiwa jinsi ya kuandaa Mpango Kazi na elimu ya uandishi wa Ripoti/Taarifa ya Utekelezaji katika Kambi ya Mafunzo elekezi kwa viongozi wapya wa mikoa 20 ya Tanzania Bara na Visiwani yanayoendelea katika Shule ya Sekondari ya Ufundi Moshi, mkoani Kilmanjaro.Taarifa zaidi ya mafunzo hayo ipo kwenye video hapo mwisho.
Victoria Mushi akifafanua jambo wakati wa mafunzo hayo.
Mshauri wa Mambo ya Sheria wa TGGA, Maria Richard akifafanua jambo wakati wa mafunzo hayo.
Baadhi ya viongozi wakifanya mazoezi kupitia michezo mbalimbali
Mkufunzi kutoka Uganda, Rita Kihembo akitoa mafunzo ya Ujasirimali kwa viongozi hao.
Viongozi wakisikiliza kwa makini wakati Mkufunzi Rita Kihembo kutoka Uganda akiendesha mafunzo ya Ujasiriamali.
Mwenyekiti wa Vijana wa TGGA Mkoa wa Arusha, Niceta Mgaya akijitambulisha alipokuwa akihamasisha wakati wa mafunzo hayo.
PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA
Mdau, nakuomba uendelee kusikiliza kupitia clip hii ya video, Victoria Mushi alielezea umuhimu wa kuandaa Mpango kazi na Ripoti sahihi, lakini pia uwasikilize viongozi waliohudhuria somo hilo wakielezea furaha yao kupata mafunzo hayo na jinsi watakavyokwenda kuyafanyia kazi watakaporejea vituoni kwao....
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...