Na Mwamvua Mwinyi, Kibaha
WAZAZI
 na walezi ,wameaswa kuacha kuhusisha watoto kwenye migogoro ya 
kifamilia pale inapotokea, kwani watoto hao bado hawana uwezo wa kubeba 
mambo ya kifamilia na masomo kwa wakati mmoja ,hali inayosababisha 
kuyumba kitaaluma.
Pia wametakiwa ,kupunguza ubize na kufuata majukumu yao ya malezi ikiwa Ni pamoja na kuwafuatilia muenendo wa masomo yao.
Rai
 hiyo ,ilitolewa na meneja wa shule za Kibaha Independent (KIPS) pamoja 
na Kibaha Annex , Nuru Mfinanga ,wakati wa mahafali ya 16 KIPS na Annex 
ikiwa ni mahafali ya kwanza ya kuwaaga wahitimu wa darasa la saba mwaka 
2021 wapatao 107.
Nuru alisema ,kwa kuhusisha mambo ya migogoro ya kifamilia majumbani inawaharibu watoto kisaikolojia.
"Tunachanganya
 watoto kisaikolojia, mwanafunzi akiwa darasani anakuwa  na mawazo yaani
 hayupo darasani kabisa ,na ukimfuatilia mtoto wa aina hii lazima 
utakuta hafanyi vizuri kimasomo"alisisitiza Nuru.
Mwenyekiti
 wa shule hizo, alhaj Yusuph Mfinanga, ameeendelea kutoa kilio chake Cha
 kuanzisha sekondari japo kuwa nia hiyo imekuwa ikikabiliwa na 
vipingamizi mbalimbali .
Alisema
 ,walishanunua shule ya Pwani sekondari kupitia mnada wa mahakama na 
matarajio ni kuigeza kuwa KIPS sekondari lakini kukatokea vizuizi kwa 
takriban miaka mitatu sasa.
"Tumekaa
 vikao ,tumeona fedha yetu tuliyonunulia hairudishwi ,na shule hiyo 
wameinunua ikiwa haina hati hivyo wameamua kuendelea na mchakato wa 
vibali vya kujenga na usajili ili mwakani shule ianze kutoa elimu 
"alisisitiza Mfinanga.
Awali
 mzazi , Abubakari Alawi alieleza, serikali ya awamu ya sita inajitahidi
 kuboresha mazingira bora ya elimu ,Anatoa wito kwa halmashauri kuanza 
maandalizi ya miundombinu mapema ili wanafunzi zaidi ya milioni moja 
2021,wanaotarajia kuingia kidato cha kwanza mwakani waingie darasani .
"Sio
 inafikia muda wa kuingia kidato cha kwanza ndio halmashauri 
zinakimbizana kuchimba msingi wa ujenzi ,lakini naimani serikali ipo 
imara kwa kuwajengea mazingira mazuri watarajiwa":;'aliongeza Alawi.
Nae
 mgeni rasmi, mkuu wa wilaya ya Kibaha, Sara Msafiri akiwakilishwa 
taarifa yake na ofisa tawala wilaya ,Asia Mwinyihaji alisema elimu 
waliyoipata wahitimu hao ,ikafungue milango ya maisha yao.
Aliwahakikishia wamiliki wa shule hiyo ,kuwapa ushirikiano katika changamoto zitakazowakabili.


 




Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...