BENKI ya NMB imezindua asasi iitwayo NMB Foundation, inayolenga kujikita katika kuimarisha uwekezaji wake kwa jamii katika sekta tano teule, sambamba na Mpango Maalum wa Udhamini wa Masomo 'NMB Nuru Yangu Scholarship and Mentorship Program’, uzinduzi uliohudhuriwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Kupitia NMB Foundation, benki hiyo inaunga mkono zaidi jitihada za Serikali kuimarisha maendeleo, ambako inaenda kuvuka mipaka ya Programu ya Uwajibikaji kwa Jamii (CSI), ambayo kwa miaka 16 ya uwepo wake, imetumia zaidi ya Sh. Bilioni 12 za urejeshaji kwa jamii kupitia asilimia moja ya faida yake kila mwaka.

Akizungumza wakati wa uzinduzi, Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB (CEO), Ruth Zaipuna, alisema asasi hiyo imejipanga kuacha alama kwa jamii ya Kitanzania, kupitia uwekezaji na urejeshaji kwa jamii kwenye sekta tano za kipaumbele ambazo ni elimu, afya, kilimo, mazingira na ujasiriamali.

Akichanganua majukumu ya NMB Foundation, Zaipuna alisema katika elimu wanatarajia kutoa misaada zaidi ya ilivyokuwa ikifanya kupitia CSI, ambako itajielekeza kukuza elimu na kuongeza idadi ya watoto wanaopata elimu, huku kwenye afya ikilenga kuboresha upatikanaji wa huduma za afya kwa makundi maalum na jamii kwa ujumla.

"Kwa upande wa mazingira, tunakusudia kuhamasisha utunzaji wake kwa lengo la kuboresha makazi ya jamii, wakati kwenye kilimo nia ni kuimarisha uwezo wa vyama vya ushirika na kuwaongezea ujuzi kupitia elimu na mafunzo ya masuala ya fedha, biashara na kuwajengea wakulima uwezo wa kukopesheka.

"Katika ujasiriamali, NMB Foundation itahakikisha inafanikisha juhudi za uzalishaji na utoaji ajira, lakini pia kukuza uchumi kwa kutoa mafunzo na uwezeshaji wa elimu ya fedha, matumizi ya dijitali, ubunifu na uendelezaji wa biashara ili kuharakisha mabadiliko chanya katika sekta hiyo, inayokusanya kundi kubwa la vijana," alisisitiza Zaipuna.


Kupitia 'NMB Nuru Yangu Scholarship and Mentorship Program,' Zaipuna alifafanua kuwa ni program ya ufadhili wa masomo kwa vijana wa ngazi ya chuo na Sekondari wanaotoka katika familia zisizojiweza, ambao utaanzia mwaka huu wa masomo wa 2021/22, wanakoratarajia kusaidia vijana 200, wakiwamo wanachuo wa shahada ya kwanza 50 na wanafunzi wa Sekondari 150 kote nchini.


Kabla ya kuzindua NMB Foundation, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliipongeza NMB kwa ubunifu uliozaa asasi na program zilizozinduliwa, ambazo ni rafiki kwa jamii, zinazoenda moja kwa moja kusapoti jitihada za Serikali katika kusimamia maeneo yote yaliyotajwa katika vipaumbele vitano vilivyoainishwa.


Alibainisha kuwa, NMB sio wageni wa kuunga mkono jitihada za Serikali kutatua changamoto za kijamii na kwamba NMB Foundation ni kielelezo cha benki inavyojitoa katika kuitendea haki jamii ya Watanzania na kuwa kupitia CSI, kwa miaka mitano iliyopita benki hiyo imeweza kuwafikia wanufaika zaidi ya milioni 5 kote nchini.


"Uzinduzi huu unaofanyika hapa una baraka zote za Serikali, kwa sababu tunatambua kuwa asasi hii ni muhimu kwa ustawi na maendeleo ya Taifa na watu wake, kama ilivyo pia kwa Programu ya NMB Nuru Yangu, ambayo inaenda kuwabeba mamia ya vijana wetu kutoka katika jamii ya wasiojiweza, ambao sisi kama Serikali tayari tumeshawekeza vya kutosha katika kuwakomboa kielimu.


"Serikali tunaahidi sapoti ya kila namna kwa NMB kutokana na jinsi inavyojitoa katika kutuunga mkono kwenye maeneo mbalimbali.


"Mchango wa NMB kwa jamii ni mkubwa unaopaswa kuigwa na wadau wengine. Serikali inatambua na kuthamini harakati chanya za benki hii, tunawaomba endeleeni kuchapa kazi, tuko nyuma yenu," alisisitiza Waziri Mkuu.


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna wakizindua NMB Foundation jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Mwanaidi Ali Khamis na Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi wa NMB, Dk Edwin Mhede





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. So amazing i am little bit ashamed to share this marvelous story about a great Dr Kham who helped me to eradicate my HSV-2, I want to write a little testimony about the good work of doctor Kham who cured me from Hsv 1 and 2 for just 2 week with his herbal medicine, I never believe I can be normal again and have a good life like others I always regretted the day I got diagnose with the virus, I was lost of hope when my doctor told me there is no cure for it but I keep thinking and thinking about my future, if I can have kids of my own well I am so grateful for my helper who get me cured with his herbal medicine, I go online in search of anything that can help me because I can’t deal with it forever so I found this doc Kham email on a blog of someone who was cured by him I quickly contact him for help and explain all my pain to him, he told me not to worry about it there is cure for real, I never believe until he send me the herbal medicine when I order for it and I have it within 4 days that is how I took the medicine for 2 week and the following week I go for test just to confirm I was 100% cured from this sickness what a miracle in my life I am so happy right now, you can also get in contact with him if you have such sickness through dr.khamcaregiver@gmail.com and also WhatsApp him +2348159922297… You can visit his website: https://herbal-dr-kham.jimdosite.com

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...