Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro amekabidhi rasmi uwenyekiti wa Shirikisho la Wakuu wa Polisi Mashariki Mwa Afrika EAPCCO na kumkabidhi uwenyekiti huo Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Congo IGP Dieudonne Bahigwa.

Hafla ya kukabidhi unyekiti huo imefanyika Oktoba 14, 2021 nchini Congo ambapo jumla ya nchi 14 wanachama wa shirikisho hilo wamehudhuria hafla hiyo ya makabidhiano. IGP Sirro ameliongoza Shirikisho hilo kwa kipindi cha miaka miwili mfululizo ambapo wakati wa uongozi wake amesaidia shirikisho hilo katika kukabiliana na uhalifu unaovuka mipaka, usafirishaji wa dawa za kulevya, ugaidi pamoja na matishio mengine ya kiusalama.
Aidha, kufuatia ushirikiano wa wakuu hao wa Polisi kumewezesha kufanyika kwa operesheni za pamoja sambamba na ubadilishanaji wa taarifa za uhalifu na wahalifu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...