Na. Dennis Gondwe, DODOMA


SERIKALI imekuwa ikipeleka fedha moja kwa moja katika vituo vya Afya ili kupunguza urasimu unaosababisha kuchelewa kwa huduma zinazotakiwa kutolewa.

Kauli hiyo ilitolewa na mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Joseph Mdachi alipokuwa akiongea na timu ya wataalam wa Kituo cha Afya Mkonze na viongozi wa Kata ya Mkonze, kikao kilifanyika katika kituo hicho.

Dkt. Mdachi alisema kuwa serikali inaleta fedha moja kwa moja kituoni. “Kwa kuwa serikali inaleta fedha moja kwa moja kituoni, changamoto ya fedha, huduma na dawa zinatakiwa kushughulikiwa katika ngazi ya kituo na kata.

Wakati huohuo, alisisitiza kina mama wajawazito kuhamasishwa kuhudhuria kliniki pale wanapojigundua kuwa wajawazito. “Mchakato wa mama mjamzito kujifungua siyo kitendo cha dharura kwa sababu kuna muda wa miezi tisa ya ujauzito. Changamoto kubwa ni wakina mama wengi wanachelewa kuanza kliniki na baadhi yao kufariki kwa kupoteza damu” alisema Dkt. Mdachi.

Alisema kuwa mama mjamzito anapohudhuria kliniki mapema anashauriwa kitaalam kuelekea kujifungua salama. “Katika kipindi hicho, kutokana na uchunguzi wa kitaalam, mama atashauriwa kama itabidi kujifungulia katika hospitali kubwa ili familia ianze kujiandaa mapema” alisema Dkt. Mdachi.

Mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Jiji la Dodoma, Dkt. Joseph Mdachi wa pili (kulia) akitoa maelekezo ya namna serikali inavyopeleka fedha katika vituo vya kutolea huduma za afya 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...