Hayo yameelezwa leo na Balozi wa Uturuki nchini Tanzania Dkt. Mehmet Gulluoglu alipofanya ziara MNH ili kuona fursa zilizopo za ushirikiano.
Amesema, Serikali ya Uturuki iko tayari kuleta waatalamu katika maeneo ambayo MNH ina upungufu ili kuwajengea uwezo hapahapa nchini na wengine wataenda nchini humo kupata mafunzo mbalimbali kulingana na mahitaji ya hospitali.“Natambua mko kwenye hatua za mwisho za kuanza kupandikiza ULOTO, hivyo ili kufanikisha kuanza kwa huduma hii, sisi tuko tayari kupeleka watalaamu wa MNH kwenda Uturuki wakaone huduma hii inavyotolewa na Hospitali kubwa zenye viwango vya kimataifa na kisha warudi nchini kuanza kutoa huduma hii,” amesema Dkt. Gulluoglu.
Amesema maelefu ya wananchi wanapata huduma kila siku MNH kupitia mawanda mapana ya huduma hizo, hivyo hospitali inahitaji kupewa ushirikiano katika nyanja hizo ikiwemo uanzishwaji wa huduma mpya za tiba, uchunguzi pamoja na upasuaji katika magonjwa mbalimbali.
Mkurugenzi Mtendaji wa MNH, Prof. Lawrence Museru amemshukuru Dkt. Gulluoglu kwa ziara yake ambayo imefungua milango ya ushirikiano na kuahidi kutumia vyema fursa zote zitakazotolewa na Serikali ya Uturuki ili kunufaisha wananchi na kupunguza mzigo kwa Serikali kupeleka wagonjwa nje kwa huduma ambazo hazijaanzishwa.
Prof. Museru akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Dkt. Gulluoglu pamoja na wakurugenzi wengine wa MNH.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...