Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Ashatu Kijaji (katikati) akizungumza na Katibu Mkuu wa Umoja wa Posta Afrika (PAPU), Sifundo Moyo ambaye alimtembelea ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma. Kulia ni Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Dkt Zainab Chaula.

Katika kikao hicho, Katibu Mkuu wa Posta Afrika, Dkt Moyo amempatia taarifa ya utekelezaji wa ujenzi wa Jengo la Makao Makuu ya Posta Afrika jijini Arusha litakalokuwa la ghorofa 17, kuwa hadi sasa ujenzi wake umefikia ghorofa 12.

Dkt. Moyo atahudhuria kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Posta Duniani kesho Oktoba 9, ambayo kwa hapa nchini yatafanyika kwenye ukumbi wa Jakaya Kikwete Dodoma na mgeni rasmi atakuwa Makamu wa Rais, Dkt Philip Mpango.
Waziri Kijaji (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu wa PAPU, Sifundo Moyo Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Dkt Chaula na maafisa wa PAPU na wizara hiyo.

Waziri Kijaji akizungumza na mgeni wake, Katibu Mkuu wa PAPU, Moyo.

Waziri Kijaji akiongoza mazungumzo na maafisa wa PAPU na wa wizara hiyo ofisini kwake Mtumba.

PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...