Na Mwandishi Maalum
JAJI Mfawidhi Kanda ya Bukoba, Mhe. Dkt. Ntemi Kilekamajenga, amesema, Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba inaweza ikawa inaongoza au ya pili kwa kuwa na kesi nyingi za mauaji.

Jaji Mfawidhi ameyaeleza hayo mwisho  mwa wiki ( Ijumaa ) mbele ya Makatibu Wakuu  Watatu waliofika  Mahakamani  hapo katika  ziara yao ya Kikazi    ya  kujionea shughuli za utoaji hakijinai zinavyotekelezwa katika  Mahakama  Kuu na Mahakama za Chini  Mkaoni  Kagera, mafanikio na  changamoto wanazokabiliana  nazo.

Kwa mujibu wa Jaji Mfawidhi Kilekamajenga,   ongezeko la kesi  za mauaji katika  Mkoa huo  ni suala linalofikirisha si kwa Mahakama peke yake    bali pia kwa wadau wengine  wanaohusika na  mnyororo  wa uotaji  haki Jinai Mkaoni  Kagera.

“Waheshimiwa Makatibu  wakuu, kwanza nitoe shukrani zangu kwa ujio wenu, haijawahi kutokea  kwa Mahakama yetu kutembelewa na Makatibu Wakuu Watatu kwa wakati moja. Nieleze kwamba moja ya  changamoto kubwa tuliyonayo ni idadi kubwa ya kesi za mauaji” Akasema Jaji Mfawishi na  kuongeza

Anaongeza kwamba,    wao kama   Majaji na Mahakama  kwa ujumla wamekuwa wakijiuliza sababu za ongezeko la visa hivyo katika Mkoa wa Kagera, Mkoa  ambao unapakana  na nchi Jirani tatu, Uganda,  Rwanda na  Burund

“Kanda ya Bukoba inaweza kuwa ya kwanza au ya pili kwa kuwa  na kesi nyingi za mauaji, inafikirisha sana kwa nini kuwa na  visa  vingi vya mauaji”. Anaeleza Jaji Mfawidhi  Kilekamajenga.

Akasema  Mahakama Kuu  Kanda ya Bukoba   hadi sasa ina kesi 249 ambazo  zipo tayari kuanza kusikilizwa na kwamba,    na kwamba  kesi  49 kati ya  hizo zitaanza kusikilizwa katika kikao maalum cha Mahakama Kuu kitakachoanza Mwezi Novemba Mwaka hu.

 Akabainisha kwamba,    uendeshaji wa kesi za mauaji pamoja na kwamba zipo complicated   lakini zinahitaji  fedha nyingi kuziendesha kulingana na idadi ya mashahidi.

Akasema ,  usikilizaji wa kesi  kumi (10), kwa mfano  unaweza kugharimu kati ya  shilingi  za Kitanzania  milioni  20 mpaka 25  kulingana  na idadi ya  mashahidi hali  inayopelekea kusikilizwa kwa kesi chache kutokana na ufunyu wa  bajeti na hivyo  kuathiri mnyororo wa uotaji haki.

 na  Akabainisha mbele ya  Makatibu hao kwamba,   usikilizaji wa kesi  kumi (10) kwa mfano , zinaweza kugharimu  karibu  shilingi  za kitanzania   milioni 20 hadi 25 kutegemeana na  idadi ya mashahidi.

“ Kesi za mauaji  ni ngumu sana  na zinahitaji  fedha nyingi sana. Tuna  kesi   249 za mauaji, lakini  zitakazoweza kusikilizwa ni 49 tu kutonana na ufinyu wa bajeti, tunaiomba  serikali  ione  namna ya  kusaidia ili   haki iweze kutendeka na kwa wakati na kupunguza msongamano usio wa lazima katika magereza yetu”. Akasisitiza Jaji Mfawidhi Imani Kilekamajenga.

Suala la  kuwapo kwa matukio ya mauaji Mkoani Kagera  halikuelezwa tu na Jaji Mfawidhi wa  Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba bali pia  limezungumwa na   Mkuu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa  Bukoba Kamishna Msaidizi  Awadhi Juma Hajji.

Akizungumzia hali hiyo,  RPC  Awadhi Juma Hajji  amesema kwa muda mfupi aliokaa  Mkoani  Kagera,  akiwa ametokeza Zanzibar amekuwa akipokea taarifa za  mauaji  na kubwa linalosababisha  matukio ya kuuana  mkoani  hapa ni  wivu wa mapenzi.

Na kwa sababu hiyo  ameshauri  kuendelea kutolewa kwa elimu kwa jamii  kuacha kujichukulia sheria  mkononi  lakini pia  kila mwananchi katika nafasi yake anapashwa kutimiza wajibu wake ili kupunguza  na kuondoa kabisa matukuo ya  mauaji katika jamii.

“ Muda mfupi  ambao nimekaa hapa nimekuwa nikipata taarifa za mauaji hali  si nzuri  sana, wajibu wetu Polisi ni kuhakikisha usalama wa wananchi na mali zao, ninaomba sana ushirikiano kutoka kwa  wananchi  na wadau wengine ya Hakijinai, na kila mmoja wetu akitimiza wajibu wetu, changamoto zinazoikabili  jamii zitapungu.Amesisitiza  RPC Hajji.

Naye  Mwendesha Mashtaka Mkoa wa  Kagera  Juma Masanja akizungumzia  hali hiyo ya mauaji Mkoani  Kagera, licha  ya kusema  visa vingine vinatisha na kushangaza kwamba mwanadamu anaweza kumfanyia hivyo mwanadamu mwenzi amewataka  Maafisa   Ustawi wa Jamii na Maendeleo  kuendelea kutoa elimu kwa wananchi  juu ya  madhara ya kujichukulia sheria mkononi.

“katika hili  na mimi  naomba nichangie, kwa kweli hali si nzuri, kesi ni nyingi, na wakati mwingine matukio mengine yanatisha na kuogofya mpaka unashangaa hivi ni mtu anaweza kufanya hivi. Niwaombe Maafisa  Ustawi wa Jamii na Maendeleo mtoe elimu kwa wananchi na muwaeleze kwamba kujichukulia  sheria Mkononi ni Kosa la Jinai” akasitiza Mwendesha Mashtaka Juma Masanja.

Mmomonyoka wa maadili,  watu  kutokuwa na hofu ya mungu, wivu wa mapenzi,  ulevi wa kupindukia, na  migogoro  ya ardhi ambayo nayo imeelezwa kuwa ni mingi  Mkoani  Kagera  ni  baadhi ya sababu zinazoelezwa kuongeza visa ya mauaji katika mkoa huo.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu  Wizara ya Katiba  na Sheria, Profesa Sifuni Mchome,  akizungumza visa hivyo, amesema takwimu za matukio hayo zinatisha na  haziendani na  Nchi ambao imeingia katika Uchumi wa Kati.

“Nchi yetu  imeingia katika uchumi wa kati, lakini bado tunafanya mambo  ambayo hayaendani na nchi  iliyoingia katika uchumi wakati, tunapashwa kama jamii kubadilika na ni wazi kuna jambo linatakiwa kufanyika kwa nini jamii imeingia katika hali hii ya  kuuanza” akasisitiza Profesa Mchome.

Makatibu Wakuu Sifuni Mchome ( Katiba na Sheria),  John Jingu ( Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na watoto) na Christopher  Kadio ( Mambo ya Ndani) wamehitimisha ziara yao ya kikazi ya wiki moja katika  mikoa ya Tabora,  Kigoma na Kagera.

Mhe. Jaji Mfawidhi wa   Mahakama Kuu  Kanda ya Bukoba, Dkt. Ntemi Kilekamajenga, akielezea  mafanikio na changamoto za utoaji haki jinai  katika  Mahakama  Kuu Kanda ya Bukoba na Mahakama za chini kwa Makatibu Wakuu watatu   Sifuni Mchome, John Jingu na Chrishopher  Kadio  ( hawapo Pichani) moja ya  changamoto kubwa aliyoilezea Jaji Mfawidhi ni uwepo wa kesi nyingi za mauaji katika mahakama hiyo, Jumla ya  Kesi 249 zimekwisha kamilika upelelezi na 49 kati ya hizo  zitaanza kusikilizwa katika kikao maalum cha Mahakama Kuu kinachotarajiwa kuanza  Mapema Mwezi   Novemba mwaka huu.
Majaji wa Mahakama Kuu  Kanda  ya Bukoba, Mhe. Jaji  Ayubu Mwenda,  Mhe. Jaji Angaza Mwipopo  na Mhe. Jaji Emmanuel Ngigwana. Mahakama Kuu  Kanda ya Bukoba ina majaji  wanne (4) pamoja na  kesi nyingi za mauaji,  Mahakama Kuu  Kanda ya Bukoba pia inamashauri mengi ya migogoro ya ardhi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...