Waziri wa Nchi Ofisi ya Raisi Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Mohamed Mchengelwa akizindua Mfumo wa maombi ya kazi kupitia simu za kiganjani uliofanyika katika ukumbi wa Tume ya Uchaguzi jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe.Mohamed Mchengelwa (wa katikati), Naibu Waziri ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deogratius Ndejembi (wa pili kushoto), Katibu Mkuu Utumishi na Utawala Bora Dkt. Laurean Ndumbaro(wa kwanza kulia), Mwenyekiti wa Bodi ya Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma Bi.Sophia Kaduma (wa pili kulia) pamoja na Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA Bw. Samweli Tanguye wakifuatilia kwa umakini mfumo wa maombi ya kazi kupitia simu za kiganjani kwenye screan za ukumbi.
Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma Bw. Xavier Daudi akitoa hotuba yake mbele ya Mgeni Rasmi kwa kuelezea namna ambavyo mfumo utafanya kazi na kuwasaidia waombaji fursa za ajira nchini.
Baadhi ya washiriki wakiwa kwenye ukumbi wa Tume ya Uchaguzi wakishuhudia uzinduzi wa " Ajira Portal Mobile App" jijini Dodoma
Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Mohamed Mchengelwa (wa tatu kutoka kulia aliyekaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na Menejimenti ya Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma mara baada ya kuzindua Ajira Portal Mobile App.
Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Mohamed Mchengelwa (wa tatu kutoka kulia aliyekaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na Katibu wa Sekretarieti ya Ajira Bw. Xavier Daudi ( wa kwanza kulia aliyekaa) pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Sekretarieti ya Ajira mara baada ya kuzindua Ajira Portal Mobile App.
Waziri, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Mohamed Mchengelwa (wa tatu kutoka kulia aliyekaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na Naibu Waziri Mhe. Deogratius Ndejembi (wa pili kutoka kulia aliyekaa), Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Laurean Ndumbaro ( wa pili kutoka kushoto aliyekaa) Mwenyekiti wa Bodi ya Sekretarieti ya Ajira Bi.Sophia Kaduma (wa kwanza kushoto aliyekaa) na Katibu wa Sekretarieti ya Ajira Bw. Xavier Daudi ( wa kwanza kulia aliyekaa) pamoja na wawakilishi kutoka Mradi wa Maendeleo PS3+ mara baada ya kuzindua Ajira Portal Mobile App.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...