“Wanawake wanayo nafasi kubwa ,Ukimpa mwanamke nafasi ya uongozi ,huwa wanaongoza kwa msingi wa sheria,hivyo wakiwepo wanawake wengi viongozi nchi za Afrika lazima zitaendelea"


Na.Vero Ignatus,Arusha


Wanawake wameaswa kujitokeza na kuwa msatari wa mbele katika kuchukua nafasi mbalimbali ili kuonyesha uwezo wao na utendaji katika uongozi, kwani wanawake wakipewa nafasi huwa wanafanya kazi kwa uaminifu

Naibu Katibu Mkuu wa Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Mipango, Miundombinu, Fedha na Utawala Mhandisi Steven Mlote ameyasema hayo wakati akifungua kongamano la mtandao wa wanawake barani afrika la maendeleo na mawasiliano (Femnet) linalofanyika jijini Arusha.
Mhandisi Mlote aliwataka wanawake popote pale walipo wajione wao ni viongozi kuanzia ngazi ya familia,mikoa, Taifa pamoja na uongozi wa jumuiya,ambapo alisema Nyumba ambayo haina mwanamke hata maendeleo yanalegalega.

“Wanawake popote pale walipo wajione kama wao ni viongozi na uongozi wao isiishie kwenye familia zao bali wajitokeze kuonyesha uwezo wao katika kuongoza na sisi wanaume tuwape nafasi maana mwanamke ukimpa uongozi hana longolongo”alisema Mlote.

Mhandisi Mlote,alisema kuwa idadi ya wanawake duniani ni kubwa, hivyo haoni sababu ya wanawake kubaki nyuma katika suala la uongozi,ambapo aliwakaribisha katika jumuiya ya Afrika mashariki kuchangamikia fursa za uongozi na kuleta usawa kwa wanaume.

Nae Mratibu wa WWP Sifisosami Dube kutoka nchini Afrika ya kusini alisema kuwa, Wanawake wanaoingia katika siasa wanatakiwa kujengewa uwezo pamoja na ili waweze kufikia malengo ya kile wanachokiendea kwaajili ya jamii inayomzunguka pamoja na kuwajengea uwezo katika kufanya maamuzi,wanawake wapo tayari ila kutokana na vikwazo wanavyokutana navyo hawawezi kupiga hatua

Mwanamke yupo tayari muda wote changamoto inajitokeza pale amabapo anakosa pesa za kufanya kampeni ihawawezi kuwa na nguvu

Vilevile Spika wa Bunge la Africa Mahariki Martin Ngoga alilitaka Baraza la Mawaziri, kupendekeza kwa Wakuu wa Nchi wanachama wa Africa Mashariki, kutoa nafasi ya upekee na kua na Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki atakae shughulikia Kipekee Masuala ya Jinsia

Naye mbunge wa Afrika Mashariki kutoka Nchini Rwanda Fatuma Ndangiza,alisema usawa wa kijinsia sio suala la wanawake pekee bali ni suala la jamii Kwa kuwa changamoto kubwa ni tamaduni zetu hivyo jitihada zaidi zinahitajika katika mshikamano ili kuondoa dhana ya mfumo dume

Mhandisi Pamela Maasai ambaye ni Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) msemaji wa Umoja wa wanawake katika Bunge la (EALA,)aliwataka wanawake kutumia fursa za uongozi kuonyesha uwezo wao ili kujenga mazingira ya kuaminika kwani wanawake wengi Barani Afrika wamekuwa wakisita kugombea nafasi za uongozi,kutokana na athari za mfumo dume uliojengeka miongoni mwa Jamii.

Aidha Alisema baadhi ya wanaume wamekuwa vikwazo katika kutoa ushirikiano kwa wanawake pindi wanapotaka kugombea nafasi za uongozi wakiamini kwamba mwanamke ni kiumbe dhaifu hawezi kumwongoza mwanaume jambo ambalo limepitwa na wakati,badala yake wao ndio wanatakiwa kuwa mfano wa kuigwa kwa kuwatia moyo wanawake pale wanapoonyesha nia kuwania nafasi hizo.

Kwa upande wake mshiriki wa kongamano hilo Rose Mjilo kutoka shirika la Mimutie women kutoka jamii ya kifugaji wilayani Ngorongoro ,alisema changamoto ya mfumo dume Kwa Jamii ya kimasai bado ni kubwa hivyo elimu zaidi inahitajika ili kuikwamua jamii hiyo kuachama na dhana hiyo.

AIDHA jamii hiyo bado inaendekeza mfumo dume wa Uongozi Kwa wanawake na kutolea mfano kuwa hivi karibuni alijitosa kugombea mchakato wa kupitishwa kuwa mgombea ubunge katika jimbo la ngorongoro akiwa mwanamke pekee lakini wanaume walimbeza na kujikuta akikosa hata kura Moja.Naibu Katibu Mkuu wa Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Mipango, Miundombinu, Fedha na Utawala Mhandisi Steven Mlote,akifungua Kongamano la mtandao wa wanawake barani afrika la maendeleo na mawasiliano (Femnet) linalofanyika jijini Arusha.

Spika wa Bunge la Africa Mahariki Martin Ngoga:Wakuu wa Nchi wanachama wa Africa Mashariki, kutoa nafasi ya upekee na kua na Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki atakae shughulikia Kipekee Masuala ya Jinsia



Dkt.Rose Reuben Mkurugenzi wa TAMWA akizungumza Kongamano la mtandao wa wanawake Barani afrika la Maendeleo na Mawasiliano (Femnet) linalofanyika jijini Arusha.

Mbunge wa Afrika Mashariki kutoka Nchini Rwanda Fatuma Ndangiza: Usawa wa kijinsia sio suala la wanawake pekee bali ni suala la jamii,kila mmoja anao wajibu wa kuhakikisha napambana kwa pamoja .

Mratibu wa WWP Sifisosami Dube International Idea kutoka nchini Afrika ya kusini:Mwanamke yupo tayari muda wote changamoto inajitokeza pale amabapo anakosa pesa za kufanya kampeni ihawawezi kuwa na nguvu



Mhandisi Pamela Maasai ambaye ni mbunge wa bunge la Afrika Mashariki (EALA)“Wanawake tuache woga tujiamini na tugombee nafasi mbalimbali za uongozi hasa katika nyaja za siasa na tulipata tionyeshe uwezo wetu.



Mkurugenzi wa TAMWA dkt.Rose Reuben akifuatilia jambo kwa makini katika kikao Kongamano la mtandao wa wanawake barani afrika la maendeleo na mawasiliano (Femnet) linalofanyika jijini Arusha

 

Rose Mjilo kutoka shirika la Mimutie women :kutoka jamii ya kifugaji wilayani Ngorongoro ,alisema changamoto ya mfumo dume


Rachel Kagoya (FEMNET)nchini Kenya:
Ushiriki katika kampeni za wanawake wanaoongoza Afrika,wanawake katika kufanya maamuzi ya kisiasa,kutengeneza miongozo ya kuongeza wawakilishi wa wanawake katika siasa, Majukwaa mbalimbali yanawaunganisha wanawake wa Afrika kwa pamoja ,kwani mabadiliko wanayoyasema yamechukua muda mrefu,na wanahitaji kuwekeza zaidi ili kuleta mabadiliko chanya Barani Afrika

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...