Muonekano wa maendeleo ya ujenzi wa Chuo cha Elimu ya Biashara tawi la Mbeya kwenye eneo la Iganzo Jijini Mbeya. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa aliweka jiwe la Msingi la Ujenzi wa Chuo hicho, Novemba 30, 2021.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya , Juma Homela kuhusu ujezi wa vibanda na miundombinu mingine katika eneo jipya la wafanyabiashara wadogowadogo maarufu kwa jina la Machinga la uwanja wa ndege wa zamani wa Mbeya wakati alipotembelea eneo hilo jijini Mbeya, Novemba 30, 2021.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama kibanda nambari moja kikiwakilisha vibanda vingine vingi vya wafanyabiashara wadogowadogo maarufu kwa jina la Machinga wakati alipotembelea eneo jipya la wafanyabiashara hao lililoanzishwa na Jiji la Mbeya kwenye Uwanja wa ndege wa zamani wa Mbeya, Novemba 30, 2021.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...