JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU

Simu: 255-262961500/1 

Nukushi: 255-262961502

Baruapepe: press@ikulu.go.tz

Tovuti : www.ikulu.go.tz               


Dodoma.

09 Novemba, 2021.


Description: Description: Description: Description: Description: Coat of Arms

OFISI YA RAIS,

      IKULU, 

 1 BARABARA YA JULIUS NYERERE,   

CHAMWINO,

S.L.P 1102,

40400 DODOMA.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kesho tarehe 10 Novemba, 2021 anatarajiwa kuondoka nchini kuelekea Cairo nchini Misri kwa ziara ya Kiserikali ya siku tatu.

Ziara hiyo  ya Kiserikali ya siku tatu inafuatia mwaliko wa Rais wa nchi hiyo, Mhe. Abdel Fattah Al Sisi. 

Katika ziara hiyo, Mhe. Rais Samia pamoja na mambo mengine anatarajiwa kufanya mazungumzo na mwenyeji wake katika maeneo kadhaa ya ushirikiano kati ya Tanzania na Misri ikiwemo nyanja za diplomasia, uchumi, siasa, elimu, utalii na huduma za kijamii. 

Mhe. Rais Samia na mwenyeji wake pia wanatarajiwa kushuhudia utiaji saini mkataba mmoja (1) na hati saba (7) za makubaliano kati ya Tanzania na Misri.


Jaffar Haniu

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...