Na Khadija Kalili, Kibaha

Katibu wa Chama Cha Wafanyakazi  wa Vyombo Vya Habari Tanzania (JOWU TA) Suleiman  Msuya ametoa hamasa kwa Waandishi wa habari kujiunga na Chama hicho ambacho ni chama huru  kwa wanahabari  wote nchini  Ili waweze kutetea haki zao za msingi ambazo zimepokwa kwa miaka mingi na vyombo mbalimbali ambavyo wamekua wakivitumukia.

"JOWUTA  ambacho Mwenyekiti wake wa Taifa ni Claudio Gwangu ni sehemu sahihi kwa wanahabari  katika kutetea maslahi yao kwani haina masharti magumu ya kujiunga  ambapo pia taasisi hii imekuja katika wakati muafaka  hivyo wanahabari tuchangamkie fursa za kujiunga" alisema Msuya.

Katibu huyo wa JOWUTA aliyasema hayo wakati akifunga mafunzo ya  siku mbili kwa Waandishi wa habari yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Hoteli ya Njuweni Kibaha huku akise kuwa tayari mafunzo kama haya yameshafanyika kwenye mikoa 16 nchini na  yameweza kuamsha ari ya wanahabari wengi  kujiunga na JOWUTA.

Mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Pwani Ally Hengo alisema kuwa amefurahi kupata fursa hiyo ya mafunzo kwa wanachana wake miongoni  na kuchagiza  hamasa ya kujiunga kwani wao ndiyo walengwa wa changamoto zote wanazozipitia wanahabari.

Hengo amewashukuru  JOWUTA na kusema kuwa   anaunga mkono juhudi zao na kwamba atahakikisha anatoa hamasa  ya kutosha kwa wanahabari wengine wa  Mkoa wa Pwani kujiunga na Taasisi hiyo.

"Sisi wanahabari tunapaswa tujisemee wenyewe Sasa katika kudai haki zetu na kujijenga  kwani tumekua daraja na kuwachongea Taasisi mbalimbali kujipigania maendeleo huku sisi tukijisahau na tukikosa sauti moja ya kijisemea"alisema Hengo.

Mafunzo hayo ya siku mbili yalijikita katika kutoa elimu ya usalama masalama mahala pa kazi n usawa wa kijinsia  yamedhaminiwa na  Chama Cha Wafanyakazi Cha Wanahabari wa Norway(NORSK LAG).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...