Watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wakiendelea na zoezi la ukaguzi wa risiti za EFD katika malori ya mizigo yanayoelekea mikoa ya kusini katika eneo la Mwandege Wilaya ya Mkuranga,ambapo zoezi hilo lilianza tarehe 8 /12/2021.

Magari 21 yamekutwa na makosa mpaka kufikia leo tarehe 10/12/2021.
Meneja msaidizi wa Mkoa wa Pwani TRA Bw. Omar Chikwekwe alizungumza kwamba malori hayo yanavizia mida ya usiku kwa kuamini kuwa TRA muda wao wa kazi umeisha.

Kaika hatua nyingine Bw.Omari  amewahimiza wafanyabiashara wenye malori, wenye viwanda na wafanyabiashara wanaouza bidhaa kutokukwepa kutoa risiti kwa manufaa ya Taifa letu.

Zoezi la ukaguzi linaendelea katika njia kuu zote zitokazo Dar es Salaam pamoja na Kariakoo.

Afisa wa TRA Cosmass Mkinga (alievaa kitambulisho) akifanya usajili wa lori kwa mwenye lori eneo la Mwandege wilaya ya Mkuranga.

Afisa wa TRA (alievaa kitambulisho) Cosmass Mkinga akikagua lori eneo lq mwandege Mkuranga

Afisa wa TRA (alievaa kitambulisho) Joseph Mlimi akitoa maelekezo kwa mmiliki wa lori eneo la Mwandege wilaya ya Mkuranga

Ofisa wa TRA Cosmass Mkinga (alievaa kitambulisho) akitoa maelekezo kwa mmiliki wa lori maeneo ya Mwandege Wilaya ya Mkuranga

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...