………………………………………………….

Nteghenjwa Hosseah, OR-TAMISEMI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Ummy Mwalimu amewaelekeza Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini kuhakikisha asilimia 40 na 60 kutoka katika fedha za mapato ya ndani zinazoelekezwa kwenye maendeleo zitekeleze miradi yenye Tija.

Waziri Ummy ameyasema hayo alipokua ziarani kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Uyui kukagua miradi ya maendeleo na kukutana na Baraza la Madiwani la Halmashauri hiyo.

Akiwa Uyui amesema utekelezaji wa miradi inayotokana na mapato katika maeneo mengi mengi mara nyingi imetekeleza miradi midogo midogo ambayo haileti tija kwa haraka kwa wananchi.

‘Unakuta fedha zinapelekwa kidogo kidogo kwenye kila Kata, kiasi ambacho hakiwezi hata kukamilisha mradi mmoja mwisho wa siku miradi inabaki viporo kwa muda mrefu mpaka inaharibika na haileti faida kwa wananchi ninachotaka kuona ni fedha hizo zikitumika kwenye miradi yenye mikubwa inayoleta matokeo ya haraka’.

Aliendelea kusema nataka kuona fedha hizo zinaanza ujenzi na kukamilisha kabisa au zinakamilisha ujenzi wa majengo yaliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi ili yaanze kutoa huduma.

Tusitake kila kata fedha kidogo mwisho wa siku hakuna matokeo ya fedha mlizoweka cha msingi mkubaliane maeneo ya kimkakati mjenge miradi ikamilike na ianze kutoka huduma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...