Mwito umetolewa kwa waendesha bodaboda katika Wilaya ya Ulanga kufuata sheria za usalama barabarani na kuhakikisha wanaziepuka ajali za uzembe na kumfikisha salama abiria anayetumia usafiri huo

Wito huo umetolewa na wajumbe kamati ya usalama barabarani wilayni ulanga wakati wa uzinduzi wa wiki ya nenda kwa usalama barabarani iliyozinduliwa katika kijiwe cha bodaboda kilichopo Togo Mahenge Wilayani Ulanga

Wajumbe hao wamesema kuwa endapo kila mwendesha bodaboda atazingatia na kufuata sheria za barabarani hakutakuwa na ajali katika mji wa mahenge na wilaya kwa ujumla wake hivyo wamewataka bodaboda hao kuzingatia sheria zote za barabarani

Kwa upande wake mkuu wa usalama barabarani JOSEPH SAGALA amesema kuwa kwa mwaka huu wiki ya nenda ka usalama itafanyika kwa kuwatembelea bodaboda kwenye vituo vyao na kuwapatia elimu ya uslama barabarani ili wasio jua sheria wazijue ili kutokomeza ajali za uzembe

Mkuu huyo wa usalama barabarani amesema kuwa wameandaa vyeti vya Madereva bora kwa mwaka huu na watapatiwa vyeti wale madereva wote ambao hajawahi kupata ajali wakati wote wa kazi yao ya bodaboda

Aidha mkuu wa polisi wilayani ulanga JAKSON KAHAMBA amesema ili kutokomeza ajali wilayani ulanga amewataka bodaboda kufika ofisini kwake mara tu wanapoonewa na askari wa usalama barabarani kwani kwa kuhofia kusema ukweli itawapelekea kuzidi kuonewa nayeye asiwe na taarifa ya kuonewa kwao

Mkuu wa Polisi amesema kuwa anasikitishwa na baadhi ya Madereva wa bodaboda ambao wanaonekana kuonewa na hawasemi wanasubiri mpaka kuwe jna mkutano wa hadhara jambo ambalo hajapendezwa nalo

Akihitimisha uzinduzi huo Mwenyekiti wa kamati ya nenda kwa usalama Wilayani Ulanga Bw Christom Msakamba amewataka vijana kuhakikisha ulanga inakuwa haina ajali kwa kufuata sheria za barabarani

Nao bodaboda wameomba uongozi huo kuwapa mafunzo ya mara kwa mara na kusaidia kuwapatia leseni kwa bei nafuu,pamoja na kuahidi kupokea yale waliyopewa na kuyafanyia kazi ili kutokomeza ajali za barabarani za uzembe.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...