Na Humphrey Shao, Michuzi Tv
Afisa mtendaji mkuu wa DAWASA, Mhandisi Cyprian Luhemeja amemtaka mkandarasi anaetekeleza mradi wa Chalinze namba tatu kukamilisha mradi huo unatarajiwa kuhudumia vijiji zaidi ya 67 wilayani humo kuhakikisha wanakamilisha na kuukabidhi serikalini mradi huo kufikia tarehe 31 mwezi Machi huku akisisitiza kuwa DAWASA imejipanga kutafsiri maono na maelekezo ya Rais Samia ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na za uhakika za maji.
"Hapa tupo Chamakweza, katika mradi wa Mlandizi-Chalinze-Mboga, na kama mnavyoshuhudia mradi huu umekamilika tunasubiri kukabidhiwa tu....Mradi huu umegharimu Shilingi za kitanzania bilioni 18". Alisema Luhemeja
" Tunawapongeza sana watanzania, kwani hizi bilioni 18 kwa kweli zimetokana na makusanyo yetu wenyewe ya ndani, wanalipa ankara vizuri na kwa wakati na kutuwezesha kukamilisha mradi huu. Hongereni sana watanzania". Aliongeza Luhemeja
Aidha akizungumzia mradi wa Chalinze namba tatu Luhemeja alisema
" mradi huu umechukua muda mrefu sana. Wakandarasi wa awali waliuvuruga na sasa tunao wakandari wapya ambao kwa kweli wanaenda vizuri. Nimewaomba hapa wafanye iwavyo itakavyokuwa kufika tarehe 31 mwezi machi wawe wamekabidhi mradi huu". Alisema Luhemeja
Luhemeja alisema kuwa mradi huo unaogharimu bilioni 100 unagharamiwa kwa ushirikiano baina ya Tanzania na benki ya Exim kutoka India
"Mradi huu ni mkubwa sana na utakuwa tiba ya changamoto ya maji kwa maeneo mengi yaliyokadiriwa na upembuzi wa mradi, utahudumia zaidi ya vijiji 67'',alisema Luhemeja.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...