Na Khadija Kalili ,Pwani

Katibu Mkuu wa Chama Cha Cha Mapinduzi CCM Daniel Chongolo amefungua barabara ya Ukombozi ya Kilomota 1.8 inayokwenda Chuo Cha Uongozi Cha Siasa Cha Mwalimu Nyerere kilichopo eneo la Chang'ombe Kata ya Kwamfipa Halmashauri ya Kibaha Mjini Mkoani Pwani.

Akifungua barabara hiyo leo Komredi Chongolo amewataka wananchi wa eneo hilo la Kwamfipa kulinda miundombinu ya barabara hiyo ikiwa ni pamoja na kutumia fursa hiyo kujiimarisha kiuchumi.

"Ukombozi tunaoenda nao baada ya kufungua barabara hii ni pamoja na kujikomboa kiuchumi hivyo wito wangu kwenu wana Pwani lazima na ninyi mtengeneze programu za kujiendeleza pia muweke mifumo mizuri na yenye tija na kutumia ufunguzi wa barabara hii kwa kuwa ni muhimu sana kwenu hivyo mnao wajibu wa kuitunza " alisema Komredi Chongolo.


"Nimeona mmeanza kutupa takataka pembezoni mwa barabara hili jambo nalikemea kwa sauti kuu kwamba siyo sahihi hivyo ngazi zote za uongozi msimamie usafi wa barabara hii pamoja na kuitunza" alisema Chongolo,

Akizungumza baada ya uzinduzi huo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kibaha Erasto Mpangala alisema kuwa awali eneo hilo lilikuwa katka hali mbaya sana na haikuwa rahisi kupitika hivyo ujenzi wa barabara hiyo inayokwenda Chuo Cha Mwalimu Nyerere huku aliongeza kwa kusema kuwa kwa sasa milango imefunguka kwa wakazi wa eneo hilo kwa kuwa na muingiliano kiuchumi umekua hivyo jamii husika inapaswa kuilinda.

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji Kibaha Selina Wison ameishukuru serikali ya watu wa China pamoja na vyama rafiki vya ukombozi Kusini mwabara la Afrika kwa ujenzi wa barabara hiyo huku akiahidi kushirikiana na wananchi kutunza miundombimbinu ya barabara hiyo.

Mbunge Mstaafu wa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zainab Vulllu alisema kua wakaazi wa Pwani tunamshukuru Mungu tunasema huu ni ukombozi mkubwa sana hasa kwa kina mama kwani wao ndiyo wanufaika zaidi kwa sababu ukimuwezesha mwanamke umeiwezesha familia nzima kwa ujumla,

Wengine walioshuhudia ufunguzi wa barabara hiyo ni pamoja na wawakilishi wa makatibu wenza kutoka katika nchi zilizopo Kusini mwa Afrika ambao ni Sofia Chinengwa kutoka Chama Cha (SWAPO) Namibia, Manueli Domingo Agusto kutoka (MPLA), Fransisco Mkatlea (FRELIMO) Msumbiji,Sibongile Dasani( ANC) Afrika Kusini.


Chuo hicho ambacho kimejengwa kwa ushirikiano wa vyama vitano ambavyo vilikua katika mstari wa mbele wa kupigania uhuru Kusini mwa Afrika kitazinduliwa kesho (Jumatano) na Rais wa Jamuhuri wa Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...