Na Mwandishi Wetu

Waandaaji wa mbio za 20 za Kilimanjaro Premium Lager Marathon wametangaza vituo vitatu vya kutolea namba za kukimbilia ambavyo ni pamoja na Dar es Salaam, Arusha na Moshi.

Taarifa iliyotolewa jana Jijini Dar es Salaam ilisema zoezi hilo litaanzia Dar es Salaam katika viwanja vya Mlimani City Jumamosi Februari 19, 2022 na Jumapili Februari 20, 2022 kuanzia saa sita mchana hadi saa kumi na mbili jioni kwa siku zote mbili.

“Tunatoa wito kwa wakazi wa Dar es Salaam ambao wamejisajili wajitokeze kwa wingi kuchukua namba zao pamoja na vesti za kukimbilia kwa siku mbili zilizotengwa,” walisema waandaaji hao.

Baada ya Dar es Salaam, zoezi hilo litahamia Jijini Arusha katika Hoteli ya Kibo Palace Jumanne Februari 22, 2022 na Jumatano Februari 23, 2022 kuanzia saa nane kamili hadi saa moja kwa siku hizo mbili. 

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, zoezi hilo litamalizikia Moshi ambapo namba hizo zitatolewa katika viwanja vya Chuo Kikuu Cha Ushirika Alhamisi Februari 24, 2022 kuanzia saa sita mchana hadi saa kumi na mbili jioni, Ijumaa Februari 25, 2022 kuanzia saa nne asubuhi hadi saa kumi na mbili jioni na Jumamosi February 26, 2022 kuanzia saa tatu asubuhi hadi saa kumi na moja jioni.

 “Washiriki waliojisajili wanatakiwa kuzingatia muda wa zoezi hili katika vituo husika ili kuepusha usumbufu na zoezi likishafungwa hakutakuwa na ugawaji wa namba siku ya mashindano,” walisema waandaaji hao.
Waliongeza kuwa usajili kwa ajili ya mbio za kilomita 5 bado unaendelea kwa njia ya Tigo Pesa kwa kubonyeza *149*20# na kwamba usajili pia utafanyika katika vituo vya kutolea namba.

“Tumefunga usajili kwa ajili ya Km 42 na 21 kwani nafasi zimejaa lakini ule wa Km 5 bado unaendelea,” alisema.

Kwa upande wake Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, Irene Mutiganzi ambaye bia yake ndio mdhamini mkuu wa mbio hizi, alitoa wito kwa washiriki wajitokeze kwa wingi kuchukua namba zao tayari kwa mashindano ya wiki ijayo.

“Waandaaji wametenga muda wa kutosha wa zoezi hili la kugawa namba kwa Dar es Salaam, Arusha na Moshi kama wadhamini wakuu tunatoa rai kwa washiriki wajitokeze mapema ili kuepusha usumbufu dakika za mwisho,” alisema na kuongeza kuwa wamejiandaa vizuri kuadhimisha miaka 20 ya Kilimanjaro Marathon.

Wadhamini wa mbio za Kilimanjaro Marathon 2022 ni Kilimanjaro Premium Lager (Mdhamini Mkuu) Tigo (21km) na Grand Malt (5km).
Wadhamini wa meza za maji ni pamoja na Absa Tanzania, Unilever Tanzania, TPC Sugar, Simba Cement na Kilimanjaro Water. Wasambazaji rasmi ni GardaWorld Security, Keys Hotel, Kibo Palace Hotel, CMC Automobiles na Surveyed Plots Company Ltd (SPC) na Bodi ya Utalii (TTB).

Katika hatua nyingine, Kwa mujibu wa waandaaji wa Kilimanjaro Marathon, kwa mara ya kwanza kutakuweko na maonesho yanayojulikana kama Kili Expo (The People's Expo) ambapo wadhamini na wadau wengine wa mbio hizo watapata fursa ya siku tatu za kuonyesha bidhaa na huduma wanazotoa, maonyesho ambayo yanatarajiwa kufanyika kati ya Februari 24-26, 2022, katika viwanja vya MoCU.

"Maonyesho haya pia linakusudiwa kuwapa umma uzoefu wa muda mrefu wa mbio za Kili Marathon; pia kwa mwaka huu wanaotarajia kushiriki mbio hizo watapata fursa ya kuchukua namba zao za ushiriki eneo la chuo kikuu cha Ushirika badala ya eneo la hotel kama ilivyokuwa miaka ya nyuma”, ilisema taarifa hiyo ya wandaaji.

Mbio za Kilimanjaro Premium Lager Marathon, zinatarajiwa kufanyika Jumapili ya Februari 27, 2022, katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU), ambapo zimeandaliwa na taasisi ya Kilimanjaro Company Limited na kuratibiwa na wadau wa hapa nchini kampuni ya Executive Solutions Limite



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...