Ahaidia kutoa Elimu ya usalama Kwa Madereva wa pikipiki

  Na.Khadija Seif, Michuzi TV

WATU Wenye ushawihi katika jamii washauriwa kuheshimu na kujenga nidhamu ya Hali ya pindi wanapoteuliwa kuwa Mabalozi katika Makampuni.

Akizungumza hayo Balozi wa Kampuni ya Sunbeam yenye chapa ya pikipiki ya Hero febuari 21, Haji Manara amesema mara nyingi Kampuni zimekuwa zikitoa fursa za watu wenye ushawihi kwenye jamii kuzitangaza Kampuni hizo hivyo waonyeshe juhudi na kuwaaminisha kuwa wamefanya uchaguzi sahihi katika uteuzi huo.

Haji Manara mapema Leo, ameteuliwa kuwa Balozi wa Kampuni hiyo na kuibeba rasmi Kampeni ya "Piga gia Barabara ishangae".

Pia ahaidia kufanya kazi Kwa ushirikiano mkubwa na Kampuni hiyo Huku akisisitiza swala la kutoa Elimu Kwa madereva wa pikipiki kutumia "kofia" Kwa usalama wao na abiria Ili kupunguza Kasi ya ajali za Barabara.

Aidha,Meneja Masoko wa Kampuni hiyo ambayo mpaka Sasa imeshasambaza takribani pikipiki milioni 1 duniani,Nadah Dhiyebi amesema Kampuni ya Hero Motorcorp inaongoza Kwa kutengeneza na kuzalisha pikipiki zinazoongoza Kwa ubora duniani.

"Pikipiki zinapatikana nchi nzima Kwa Mawakala wajiosajiliwa ambapo mpaka Sasa wapo Mawakala 27 wapo Kwa ajili ya kukuhudumia."

Hata hivyo Dhiyebi ameeleza kuwa bidhaa hizo zimekuja kuwakomboa watanzania Kwa kuingiza nchini pikipiki za Hunter ambazo ni hunter 100 na kuhaidi kushirikiana na Balozi huyo mpya.

Balozi mpya wa Kampuni ya Sunbeam wa chapa yake ya "Hunter" akitambulisha pikipiki aina ya "chombo ya Mishe" mara baada ya kutambulisha rasmi kuwa Balozi na kuhaidi kushirikiana nao katika kuhakikisha wateja wanapata vitu vizuri Kwa Mazingira halisi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...