Na Khadija Kalili, Pwani 

Meneja TARURA Leopold Minja amesema kuanzia Machi Mosi Mkoa wa Pwani utaanza kutumia makusanyo ya maegesho ya magari kwa Njia ya kieletroniki na utaratibu huo utatumika kwa utaratibu wa kisheria kwa kuzingatia kanuni za barabara.

TARURA kwa Mkoa wa Pwani  tuna mashine Bagamoyo na kwa.mwezi tunakusanya zaidi ya Mil.1 na kwa miezi sita tayari  tumekusanya zaidi ya Mil.17 kwa kupitia  mfumo huu hatutegemei mtu kukwepa kulipa ushuru.

Mapato yetu 2020/21 mapato yetu kwa mwaka  yalikua Mil 70 lakini kwa mfumo huu mpya tunategemea kukusanya kiasi cha Mil 100.

Alisema kuwa katika eneo la Zegwreni kunajengwa barabara ambayo itahudumia magari mazito, barabara zilizojengwa ni  Lulanzi na katika eneo korofi la Kiwanda Cha Viuatilifu.

Pia wanajenga barabara ya kutoka.Muholo kwenda Mbuchi.

Mkuu wa Kitengo  TEHAMA TARURA Stanley Mlula  alisema.mfumo huu umeondoa ulipaji wa kutumia fedha mbichi ambapo hivi Sasa kutakuwa na siku 14 za kulipa.malimbikizo ya pesa za maegesho pia  tozo ya faini imepunguzwa kutoka 50,000 ya zamani ambapo hivi Sasa fine itakuwa ni kiasi cha Sh.10,000 tukikushika ukiwa hujalupa.utalipa deni letu na  na hiyo fine pia tumejipanga kushirikiana na Vyombo vya Usalama kama Jeshi la Polisi ili kuweza kulisimamia  zoezi hili endelevu.

Ushuru huu utakuwa ukichukuliwa katika maeneo tengefu ya TARURA huku akitoa angalizo kuwa siyo sahihi kwa mtu kutizwa tozo nje ya eneo tengefu (Road Reserve).

Uzinduzi huo umefanywa na Mkuu w Mkoa wa Pwani Alhaj Abubakari Kunenge huku akianisha faida kubwa ya kwanza ikiwa ni ukusanyaji wa mapato na kutoa taarifa sahihi za mlipaji na kuondoa uwezekano wa upotevu wa makusanyo ya ushuru wa maegesho.

Meneja wa TARURA Leopold Minja akifafanua jambo katika kikao hicho.
Baadhi ya wataalam waliohudhuria uzinduzi huo.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani  Alhaji Abubakar I Kunenge amara baada ya kufanya uzinduzi huo.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...