Na Khadija Kalili, Kibaha

Mkuu wa Mkoa Pwani Alhaji Abubakar Kunenge amesema kuwa ni wajibu wa Serikali kupanga miji  huku lengo kuu likiwa ni katika kuvutia wawekezaji kuwekeza Mkoani hapa.

RC Kunenge alisema hayo leo wakati alipokuwa Mwenyekiti wa kikao Cha Baraza  Biashara katika kikao  kilichofanyika.kwenye Ukumbi uliopo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani nakuhudhuriwa na Wakurugenzi kutoka katika Halmashauri  Wakuu wa Wilaya, wafanyabiashara pamoja  na Wakuu wa Idara mbalimbali ndani ya Mkoa wa Pwani.

"Tumejipanga  kupanga maeneo yote ya  Ili tuweze kwenda sambamba katika mpango mzima wa kupanga miji Ili iweze  kufahamika vyema yalipo maeneo ya viwanda na makazi ya watu Ili kuweza kuzikwepa atharizinazoweza kuletwa na kuwepo kwa viwanda katika maeneo ya makazi ya watu" aliseme RC Kunenge.

Kunenge aliongeza kwa kusema kuwa"Tutayapanga maeneo tuliyonayo Ili yaweze  kukaa katika mpangilio mzuri na itakayowavutia wawekezaji pamoja na kutunza mazingira.

Alizungumza  hayo leo asubuhi katika mkutano wa baraza la uwezeshaji la wafanyabiashara.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kibaha Mhandisi Mshamu Munde alisema alichangia mada kuhusu suala la upimaji  alisema kuwa tayari wamepata  Bil.1.5.88 kwa ajili  ya utambuzi wa maeneo ya viwanja.

"Tumekamilisha  kupima katika eneo la kidimu  na Lulazi yaliyopo katika eneo la Kata ya Pangani Kibaha Mkoani Pwani huku lengo letu likiwa kukamilisha viwanja 20,000"alisema Mkurugenzi huyo.

Wakati huohuo  Mkurugenzi wa Halmashauri ya Chalinze Mheshimiwa Ramadan Possi.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...