Na Mwandishi Wetu
WATUMISHI wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA), wametakiwa kuthamini kazi ya kutoa huduma ya Majisafi na usafi wa Mazingira kwa wateja na kuitenda kwa ufanisi mkubwa.

Akiongea katika kikao kazi cha wafanyakazi wote kilichofanyika hivi karibun, Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA Mhandisi Cyprian Luhemeja, amesema huduma ya maji ni huduma takatifu hivyo kila mtumishi anapaswa kufanya wajibu wake ma kwa uaminifu mkubwa.

"Sote tunapaswa kuelewa kwamba kufanya kazi katika Sekta ya maji ni kwa kusudi maalum na sio kwa bahati mbaya, hivyo kila mtumishi ana mchango sahihi katika kukuza maendeleo ya Mamlaka" alisema Mhandisi Luhemeja.

Ameongeza kuwa kila mtumishi wa Mamlaka analo jukumu la kutengeneza mazingira mazuri ya kuishi kwa wakazi wa Dar es Salaam na Pwani kupitia huduma ya majisafi kwa kuhakikisha upotevu wa maji unadhibitiwa ili kuboresha upatikanaji wa maji kwa wateja.

Amesema, kuwa udhibiti wa upotevu wa maji unasaidia Mamlaka kuokoa mapato yanayokosekana ya kuwezesha kuboresha huduma.

Kikao kazi hicho ni cha kwanza tangu kuanza Mwaka 2022 kilicholenga kufanya tathimini ya utendaji kwa mwaka uliopita.
Wafanyakazi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA), wakikagua mita ya mteja wao katika kampeni ya kukusanya madeni kwa wateja mbalimbali wa mamlaka hiyo katika jijini la Dar es Salaam.
Mfanyakazi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA), akisoma mita ya mteja katika operesheni ya kukusanya madeni inayoendelea ambapo mamlaka hiyo imewataka wananchi kulipia huduma ya maji ili kuiwezesha kutoa huduma bora zaidi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...