Na.Khadija Seif, Michuzi Tv

KAMPENI ya ugawaji wa taulo za kike Kwa baadhi ya shule iliyoandaliwa na Shirika la Bima Zanzibar (ZIC) lahitimishwa rasmi  katika wiki ya Kuadhimisha Siku ya Wanawake Dunia Mkoani Arusha.

Akizungumza na wanafunzi pamoja na walimu ,Kaimu Katibu Mkuu wa Shirika la Bima la Zanzibar (ZIC) Mkoa wa Arusha ,Asha Rashid mara baada ya kutembelea shule ya Sekondari Arusha girls amesema ni muhimu jamii inayomzunguka mtoto wakike iwe chachu na silaha ya kumjengea uwezo na Mazingira rafiki  Binti na kujiona wa fahari pale anapokuwa kwenye Hedhi Ili aweze kujiamini.

"Hedhi sio ugonjwa Wala sio kitendo Cha aibu hivyo ni muhimu jamii ikatambua kuwa wanayohaki ya kuhakikisha binti huyo anajikubali na kuendelea na Majukumu yake ya kimasomo Huku ikimuhakikishia anapata taulo Kwa mlengo wa kujihifadhi kabidhi taulo za Kike awapo  shuleni."

Aidha,kaimu huyo ameeleza lengo la kuchagua shule ya Sekondari ya Arusha girl amesema ni Kutokana na kuwepo uhitaji wa taulo hizo hususani Mabinti wanapokua shuleni Shirika hilo limewiwa kutoa zawadi hizo Kwa wanafunzi hao.

Hata hivyo mbali na kutoa zawadi hizo Shirika hilo lilitoa  Elimu kwa Mabinti hao kuhusu Hedhi Salama pamoja na kuvunja upendeleo Ili kuleta Mabadiliko (Bias) katika Taifa letu na kuhakikisha Kila Binti anafikia Malengo.

Kaimu Katibu wa Shirika la Bima la Zanzibar (ZIC) Tawi la Arusha Asha Rashid akimkabidhi Mwanafunzi wa shule ya Sekondari Arusha girls box la taulo za kike mara baada ya kumaliza Kampeni ya uongozi wa Shirika hilo kutembelea baadhi ya shule za Sekondari nchini kugawa taulo kama sehemu ya Kuadhimisha Siku ya Wanawake Dunia.
Picha ya pamoja ya uongozi wa Shirika la Bima la Zanzibar (ZIC) wakiwa na Katibu wa Shirika hilo Asha Rashid wakiwa katika shule  ya Sekondari Arusha girls mara baada ya kukabidhi taulo za kike wakisikiliza machache kutoka Kwa wenyeji wao

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...