Na.Khadija Seif, Michuzi TV
MSIMU wa tatu wa Mkali wa jiko wazinduliwa rasmi jijini Dar es salaam wanawake watakiwa kuchangamkia fursa hiyo katika Sekta ya Upishi.
Akizungumza na Waandishi Wahabari Muandaaji wa Shindano hilo Zainab Issa amesema Msimu huu utakua watofauti kutokana na kuongezeka Kwa Mikoa ya kushiriki katika Shindano hilo kutokana na watu wa Mikoani kuonyesha muamko wa kuhitaji Shindano.
"Msimu huu itajumuisha Mikoa minne ikiwemo Dodoma,Tanga,Arusha pamoja na Mkoa wa Dar es salaam ."
Hata hivyo amesema sababu za Mikoa hiyo kushirikishwa kutokana na Misimu iliyopita waliweza kukusanya washiriki wengi hivyo imeleta Muamko Kwa wapishi hususani wa Majumbani kuonesha ujuzi wao Kwa Mikoa mi tatu mingine.
Aidha amewaomba Wapenzi wa kipindi hiko cha "Mkali wa jiko" kuendelea kufatilia matangazo mbalimbali Ili kujua Mkoa husika watafika lini Kwa ajili ya usahili na Kwa zawadi ya Mshindi itakua Cheti Cha kutambua ushiriki wake,Fedha pamoja na zawadi nyingine nyingi.
pia akaongeza kuwa Kipindi hiko rasmi kitaanza Mei 7 mwaka huu na kitarushwa Mubashara katika chaneli ya UTV .
Muandaji wa Tamasha la"Mkali wa jiko " Zainab Issa akizungumza na Waandishi Wahabari mara baada ya kuzindua rasmi Msimu wa 3 wa Shindano hilo Jijini Dar es salaam na Kuwahimiza wanawake hususani wa Majumbani kujitokeza katika usahili
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...