Na Amiri Kilagalila,Njombe
MAHAKAMA ya hakimu mkazi Njombe imemuhukumu Fadhili Ngoho (25) mkazi wa Ulembwe halmashauri ya wilaya ya Wanging'ombe mkoani Njombe kwenda jela kifungo cha maisha baada ya kukutwa na hatia ya kumbaka mtoto wa miaka 8.

Mahakama imebainisha kuwa kesi No 193/2020 ilikuwa ikimkabili mshtakiwa Fadhili Ngoho ambaye amehukumiwa kifungo cha maisha baada ya kumbaka mtoto wa miaka 8 ambaye ni mtu na mtoto wake wa kumlea/mtoto wa kambo aliyekuwa akisoma katika moja ya shule ya msingi iliyopo katika kata ya Ulembwe

Inaelezwa kuwa siku hiyo mshtakiwa alimbaka mtoto huyo na kumwambia asipige kelele.

Mnamo tarehe 23/2/2020 mama wa mtoto huyo alimuona mwanae hatembei vizuri ndipo alipomuuliza ana tatizo gani na kisha binti huyo akamwambia mama yake kuwa baba yake wa kambo alimbaka

Tarehe 24/2/2020 mama yake alikwenda kwa mtendaji wa kijiji kutoa taarifa juu ya tukio hilo na alipewa barua ya kwenda polisi, mama huyo alifanya hivyo na taratibu za kumpeleka hospitali mtoto ziliendelea.

Hukumu hiyo imesomwa mbele ya Hakimu mfawidhi wa mkoa wa Njombe Liad Chamshana huku ikiendeshwa na wakili wa serikali Andrew Mandwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...