Na Farida Mangube ,Michuzi TV Morogoro
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martin Shigela amelitakashirika la ugavi wa Umeme Tanzania Mkoa wa Morogoro (TANESCO) kuhakikisha linaongeza kasi ya ujenzi wa kituo cha kupoza umeme cha Ifakara ili kukipunguzia mzigo Kituo cha kupoza umeme cha Msamvu.
Shigela ameyasema hayo kutokana na kituo cha Msamvu kupata hitilafu ya tangu tukio la kituo hicho kuwaka moto Mwezi Agasti mwaka jana
Shigela metoa rai hiyo baada ya moja ya transfoma kubwa katika kituo cha Msamvu Manispaa ya Morogoro leo majira ya mchana kupata hitilafu na kuwaka moto.
Shigela amesema Transforma iliyopata hitilafu na kuwaka moto ni moja na kwamba ililetwa baada ya tukio la moto la mwaka jana huku chumba cha kuendesha mitambo kituoni hapo.
Amesema chumba cha mitambo hakikuungua katika tukio ndicho kimewaka moto, ndipo akatoa rai kwa TANESCO kufanya jitihada za makusudi kudhibiti kutokea kwa ajali ya moto mara kwa mara katika kituo hicho..
Meneja wa TANESCO Mkoa wa Morogoro Mhandisi Fedgrace Shuma amesema kwasasa bado wataalamu wanafanya tathimini kubaini kiwango cha madhara yaliyojitokeza pamoja na kufanya jitihada za kurejesha huduma ya umeme katika maeneo yaliyoathirika.
Maeneo yaliyo athirika kutokana na hitilafu hiyo ni maeneo yote ya mji wa Morogoro na kwamba huduma ya umeme itarejea kupitia kituo cha umeme cha Chalinze.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...