Na WAF - Dodoma.

Mkurugenzi wa Huduma za Tiba kutoka Wizara ya Afya Dkt. Omary Ubuguyu ameagiza kliniki za magonjwa yasiyoambukiza nchini kuwa na utaratibu wa kuwachunguza pazia la macho (Retina) wagonjwa wa Saratani.

Dkt Ubuguyu amesema hayo leo alipokuwa katika Hospitali ya Benjamin Mkapa akizindua Mpango wa Kuzuia Madhara ya Kisukari kwenye Macho.

"Kila mgonjwa mpya wa Kisukari ni lazima apimwe macho kuona hali ya pazia la jicho (Retina) kwa wakati huo likoje na yule ambaye hana changamoto basi angalau na apimwe mara moja kila mwaka" amesema Dkt. Ubuguyu.

Dkt. Ubuguyu amesema kuwa Tanzania inakadiriwa kuwa takriban asilimia 5.7 ya watu wenye umri wa miaka 20 hadi 79 wana ugonjwa wa kisukari. Tafiti zilizofanyika hapa nchini zimeonyesha kuwa asilimia 35 ya watu wenye kisukari wana madhara ya ugonjwa kwenye macho na asilimia 1 ya watu hao hupata ulemavu wa kutokuona au uoni hafifu

Dkt. Ubuguyu amesema kuwa Wizara ipo kwenye mkakati wa utoaji mafunzo kwa watoa huduma ngazi ya huduma ya msingi ili waweze kutoa huduma stahiki kwa wateja wenye magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo uchunguzi wa madhara ya Kisukari kwenye Macho (Diebetic Retinopathy)

Aidha Dkt. Ubuguyu amemshukuru Dkt. Rosemary Brennan ambaye ni Daktati Bingwa kutoka Hospitali ya Raigmore kutoka Scotland pamoja na wadau wote nchini waliofanikisha kupatikana kwa kamera maalum kwa ajili uchunguzi wa madhara ya kisukari kwenye macho.

Muuguzi wa idara ya macho katika Hospitali ya Benjamin Mkapa akimpima macho mgonjwa kwa kutumia kamera ya kisasa ya kupima retina ya macho.

Daktari bingwa mshauri wa macho kutoka Hospitali ya Raigmore Dkt. Rose Brennan akionesha kamera ya kupima retina ya macho mbele ya Mkurugenzi wa huduma za kinga Dkt. Omary Ubuguyu na Mkurugenzi mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa Dkt. Alphonce Chandika.

Meneja mpango wa taifa wa huduma za macho Dkt. Bernadetha Shilio akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa mpango wa kuzuia ulemavu wa kutokuona unaoweza kuletwa na madhara ya ugonjwa wa kisukari.

Mkurugenzi wa huduma za tiba wa Wizara ya afya Dkt. Omary Ubuguyu akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi mpango wa kuzuia ulemavu wa kutokuona uliozinduliwa katika Hospitali ya Benjamin Mkapa jijini Dodoma.

Daktari bingwa mshauri wa macho kutoka Hospitali ya Raigmore Dkt. Rose Brennan akifafanua jambo mbele ya Waandishi wa Habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa mpango wa kuzuia ulemavu wa kutokuona unaoweza kuletwa na madhara ya ugonjwa wa kisukari kwenye macho utakaotekelezwa kanda ya kati uliofanyika katika Hospitali ya Benjamin Mkapa jijini Dodoma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...