Na Mwandishi Wetu
KATIKA kuhakikisha  jamii ya watanzania inaendelea kupata habari za sayansi, teknolojia  na ubunifu Wahariri wa vyombo vya habari mbalimbali  nchini  kuendelea kutoa ushirikiano na serikali kupitia Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) lengo likiwa ni kuongeza tija eneo la Sayansi, Teknolojia na Ubunifu na (STU).

Ahadi hiyo wameitoa jijini Dar es salaam wakati wa warsha ya mafunzo ya kutazamia nafasi ya wahariri katika uzalishaji na usambazaji wa habari za sayansi, teknolojia na ubunifu iliyoandaliwa  na COSTECH kupitia kurugenzi ya Menejimenti ya Maarifa (DKM) COSTECH ili kutengeneza mkakati madhubuti utakaosaidia kuzalisha na kusambaza makala nyingi zaidi za mafanikio ya miradi mbalimbali inayotekelezwa nchini ili wananchi wafahamu kazi kubwa inayofanywa kwa ajili ya maendeleo ya Taifa.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH, Dkt. Bugwesa Katale akifungua mafunzo hayo amesema kwamba COSTECH ni  taasisi y umma na moja ya jukumu lake kubwa ni kuishauri Serikali pamoja na kuratibu na kuendeleza sayansi, teknolojia na ubunifu hapa nchini, kwa kuandaa agenda za utafiti za Utafiti na uandaaji wa nyaraka mbalimbali za namna ya kuongoza tafiti na bunifu zinaweza kuendeshwa hapa nchini.

“Leo tuko hapa katika kuhakikisha tunaendeleza jukumu la kusambaza habari za sayansi, teknolojia na ubunifu na ubinifu. Vilevile Tume ina Kurugenzi nne ambazo ni Usimamizi na Kurugenzi ya Uendelezaji wa Tafiti, Kurugenzi ya Menejimenti ya Maarifa, Kurugenzi ya Huduma za Taasisi na Kurugenzi ya Uhawalishaji wa Teknolojia na zinafanya kazi pamoja ili kuhakikisha tunapata matokeo,”.

Dkt. Bugwesa ameongeza  pia Tume ina vitengo vinavyosaidia utekelezaji wa kazi zake na mojawapo ni Mfuko wa Taifa wa Uendelezaji Sayansi na Teknolojia (MTUSATE) kazi yake kubwa ni kufadhili miradi ya utafiti na ubunifu nchini.
 
Awali Kaimu  Mhariri wa Gazeti la Habarileo Mgaya Kingoba, ameipongeza Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kwa kuandaa mafunzo hayo kwa wahariri kwani yamewajengea uwezo mkubwa kuelewa na kuongeza COSTECH ni wadau muhimu na wanamchango mkubwa kuhakikisha habari zinatoka .

Amewashauri  COSTECH waendelee kuwashirikisha waaandishi wa habari na wahariri ili waweze kutoa taarifa katika lugha rahisi wananchi waweze kuelewa dhana nzima ya matumizi ya tafiti.

Kwa upande wake, Shamuna  Said ambaye ni  Mhariri wa Habari kutoka kitengo cha Habari na Matukio TBC aliwapongeza COSTECH na kuongeza kuwa mafunzo hayo yana manufaa zaidi ambapo yataenda kutoa habari kwa lugha rahisi na kutatua changamoto ya bunifu na matokeo ya tafiti kubaki kwenye makabati bila kuwafikia walaji wa mwisho ambao ni wananchi.

“Haya mafunzo ni muhimu kwa sisi wahariri tunaozalisha vipindi na habari mbalimbali ili bunifu na tafiti ziweze kuwafikia walengwa ambao ni wananchi” amesema.

Kabla ya kufunga mafunzo hayo, Mkurugenzi wa Menejimenti ya Maarifa kutoka COSTECH, Dkt. Philibert Luhunga aliwashukuru wahariri kwa kushiriki kikamilifu katika mafunzo hayo na kusisitiza kuja na mkakati shirikishi utakaosaidia kuendeleza ushirikiano baina yao ili kufikia matamanio ya kuendesha Taifa kwa sayansi na teknolojia na hatimae kufikia maendeleo kwa ufanisi mkubwa ili jamii ya Kitanzania inufaike kwa tafiti pamoja na bunifu.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH Dk.Bugwesa Katale(wa kwanza kulia waliokaa),maofisa wa tume hiyo pamoja na wahariri kutoka vyombo mbalimbali vya habari wakiwa katika picha ya pamoja
Baadhi ya wahariri wa vyombo vya habari wakiendelea na majadiliano kuhusu ni kwa nmna gani watashirikiana na COSTECH katika habari zinazohusu Sayansi,Teknolojia na Ubunifu
Sehemu ya wahariri wakiendelea kujadiliana wakati wa mafunzo yaliyoandaliwa na CHOSTECH kwa lengo la kuweka mikakati ya pamoja ya ushirikiano ili umma wa watanzania upate habari zinazohusu sayansi,teknolojia na ubunifu
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...