Makambako

Jamii nchini imeombwa kuwasaidia wanafunzi wa kike wanaoishi katika mazingira magumu kwa kuwawezesha taulo za kike ili waepukane na adha ya kukosa masomo pindi wanapokuwa katika siku zao (hedhi)

Wakizungumza mara baada ya kupokea msaada huo, wanafunzi wa shule ya msingi Kitandililo iliyopo halmashauri ya mji wa Makambako mkoani Njombe mara baada ya kukabidhiwa taulo za kike na nguo za ndani na kikundi cha chagua kurudisha tabasamu ambazo watatumia kwa kipindi cha miezi sita,wamesema wengi wao wamekua wakishindwa kufika shule pindi wanapokuwa hedhi kutokana na kukosa vifaa vya kujisitiri na kusababisha kuchekwa na wezao.

Mwalimu mkuu shule ya msingi Kitandililo Fatuma Kimbwanda amesema kutokana na wanafunzi hao kukosa taulo imesababisha wengi wao kutumia vitambaa ambavyo si salama kwa afya zao na kuwalazimu kutohudhuria masomo pindi wanapokua hedhi.

Awali wakikabidhi taulo hizo za kike na nguo za ndani kwa wanafunzi hao wanaoishi katika mazingira magumu shule ya msingi Kitandililo wanachama wa kikundi cha chagua kurudisha tabasamu akiwemo mwenyekiti wa kikundi hicho Dafroza Kyando na Loyce Kaunda wamesema lengo lao ni kuhakikisha watoto wa kike ambao wanaishi katika mazingira hatarishi wanasaidiwa ili waweze kuhudhuria shule kama ilivyo kwa wanafunzi wengine.

Utafiti ambao umefanyika mwaka 2015 na shirika la Netherlands development pamoja na Tanzania water sanitation network katika halmashauri  za sengerema,Mufindi,chato na temeke ulionyesha asimilia 48 ya wanafunzi wa kike hukosa masomo wanapokuwa hedhi.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...