Muonekano wa Bandari ya Dar es Salaam..

 

Muonekano wa Bandari ya Dar es Salaam...
Muonekano wa Bandari ya Dar es Salaam...


*Meli kubwa ya MERIDIAN ACE

MELI kubwa ya shehena ya magari inatarajia kuwasili kwenye bandari ya Dar es Salaam. Meli hiyo kutoka Japan na Singapore itawasili Dar es Salaam Mei 9, 2022 ikiwa na magari 4397 idadi ambayo haijawahi kufikiwa kwa pamoja. Hii ndio rekodi kubwa kuliko zote. Rekodi ya mwisho ilikuwa magari 4041 yaliyowasili Aprili 08 2022.



Taarifa iliyotolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Masoko na Uhusiano wa TPA Bw. Nicodemus Mushi imesema, mafanikio hayo ni matokeo ya kazi kubwa ya kutangaza Uwezo wa Bandari za Tanzania, inayofanywa na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan na Serikali ya Awamu ya Sita kote ulimwenguni.

Amesema uwekezaji mkubwa umefanywa na Serikali katika Vitendea kazi na Maboresho ya Miundombinu ya kibandari sambamba na Kampeni za Kimasoko na ushirikiano thabiti wa TPA, wateja na wadau wake wengine.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...