Na Mwamvua Mwinyi,Kibaha Vijijini
NAIBU Waziri ,ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia kazi , vijana na ajira Patrobas Katambi, ameiagiza Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) Wilaya na Mikoa , kuingia mara moja katika ufuatiliaji na kuchunguza miradi iliyokutwa na dosari kubwa wakati Mwenge wa Uhuru ulipopita kwenye Maeneo Yao.
Aidha ameipa salamu mikoa na wilaya kutochukulia mzaha ukaguzi wa mbio za mwenge ,kwani Wizara na Serikali ipo kuhakikisha mwenge huo unatekeleza adhma na falsafa ya kuanzishwa kwake.
Akitoa maagizo hayo Shule ya msingi Mtongani ,Halmashauri ya wilaya ya Kibaha , Mkoani Pwani ,wakati alipojumuika kama Wizara yenye dhamana ya kuratibu mbio za Mwenge wa Uhuru aliitaka TAKUKURU kuchukua hatua ya haraka ili taratibu nyingine zifuate.
VILEVILE aliagiza, miradi iliyokutwa na kasoro ndogondogo kwenye mwenge na kutolewa maelekezo, Wizara inasihi Mamlaka zote katika Maeneo yanayohusika kufanya marekebisho haraka ili wananchi waweze kufaidika.
Naibu Waziri huyo aliziasa ,wilaya na mikoa ambazo bado hazijapitiwa na Mwenge kujiandaa na zihakikishe zinafuata maagizo wanayopewa .
Katambi aliwaasa ,kufuata maelekezo watakayopewa na kukubali kukusolewa na ambae atakaebainika kuikatisha tamaa timu ya vijana wakimbiza Mwenge Kitaifa hawata fumbiwa macho.
"Nawapongeza wakimbiza mwenge Kitaifa mnafanya kazi kubwa,hamlali,mpo kazini ,nawapongeza Sana;"
"Nipo hapa kwa niaba ya Waziri Mkuu, toeni ushirikiano kwa vijana Hawa sita,wameagizwa kufanya kazi na Rais Samia Suluhu Hassan, Hadi Sasa wameshafikia siku 36, wameshapitia miradi 284 yenye thamani ya sh.Bilioni 69.2";! alifafanua Katambi.
Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Kibaha, Sara Msafiri alisema viongozi wa mbio za mwenge wapo vizuri katika ukaguzi
Sara alisema ,vijana hao wanaofanya kazi kubwa na kwa
mwendo huo kutakuwa na mabadiliko makubwa ya taarifa ya mdhibiti na
mkaguzi wa hesabu za Serikali.
Awali
akipokea mwenge wa Uhuru kutokaHalmashauri ya Mji wa Kibaha,
mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Kibaha ,Butamo Ndalahwa alisema
Mwenge ukiwa Katika Halmashauri hiyo utatembelea miradi 12 yenye thamani
ya Bilioni 2.2.
Butamo
alitaja baadhi ya miradi inayotembelewa na Mwenge wa Uhuru kuwa ni
pamoja na , kuzindua madarasa ya sekondari Disunyara, kuweka jiwe la
msingi Shule ya sekondari Kikongo, mradi wa maji MinaziMikinda,ujenzi wa
kituo cha afya Kwala na kutembelea kiwanda cha Animal Care co.Ltd.
Kiongozi
wa mbio za mwenge Kitaifa,Sahir Geraruma alieleza ,Mwenge Ni jicho la
Rais kumulika utii wa sheria namna gani wananchi wanapewa huduma .
Alibainisha,
unapita kukagua na kuhakikisha ubora wa miradi na thamani ya
zinazotolewa na Serikali kutekeleza miradi mbalimbali ya kimaendeleo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...