Na Amiri Kilagalila,Njombe

Mahakama ya wilaya ya Makete mkoani Njombe imemsomea shtaka la ubakaji kijana Faison Alimajani Sanga (19) mkazi wa kijiji cha Makwaranga kata ya Ipelele anayetuhumiwa kutekeleza kosa hilo kwa mwanafunzi wa shule ya msingi wilayani humo anayetajwa kuwa na umri wa miaka 15

Mahakama imeeleza kuwa mtuhumiwa ametenda kosa hilo la ubakaji kinyume na kifungu cha 130 (1) (2) e na 131 (1) ya kanuni ya adhabu sura ya 16 marejeo 2019.

Kwa upande wa mashaidi wawili wa mashtaka akiwemo muhanga mwenyewe amesema kuwa mnamo tarehe 12 Februari, 2022 mshtakiwa alimpeleka nyumbani kwake na kufanya kitendo hicho huku akimuahidi ya kuwa atamuoa.

Shahidi wa pili ambaye ni baba wa mtoto huyo amesema kuwa alipogundua binti yake ni mjamzito na kuamua  kumpeleka kwenye kituo cha afya kwa ajili ya vipimo  na ndipo alipo gundulika ni mjazito 

Aidha mshtakiwa amekana kutenda kosa hilo na kurejeshwa rumande mpaka tarehe 30.5.2022 kwa ajili ya kuendelea kusikilizwa Tena.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...