Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango akitoa tuzo za Sayansi kwa washindi mbalimbali  wakati wa ufunguzi wa mkutano wa 31 wa pamoja wa Sayansi ulioandaliwa na  Taasisi ya Taifa ya utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) unaofanyika katika kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere Jijini Dar es salaam.

……………………

 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango akizungumza na washiriki wakati wa ufunguzi wa mkutano wa 31 wa pamoja wa Sayansi ulioandaliwa na  Taasisi ya Taifa ya utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) unaofanyika katika kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere Jijini Dar es salaam.

…………………

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango leo tarehe 17 Mei 2022 amefungua mkutano wa 31 wa pamoja wa Sayansi ulioandaliwa na  Taasisi ya Taifa ya utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) unaofanyika katika kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere Jijini Dar es salaam. Mkutano huo unashirikisha wataalamu na wadau mbalimbali wa sekta ya afya kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya Tanzania.

Akizungumza na washiriki wa mkutano huo Amesema Tanzania inaunga mkono na kuamini katika ufanyaji wa tafiti zitakazokabiliana na changamoto za maradhi hapa nchini. Ameongeza kwamba mkutano huo ni fursa ya aina yake kwa wanasayansi wa Tanzania  kujifunza kutoka kwa kila mmoja na kuunganisha werevu na uwezo katika kupata masuluhisho ya kimsingi kwa changamoto kuu za kiafya hapa nchini.

Makamu wa Rais amesema mkutano huo una umuhimu mkubwa kutokana na kufanyika katika kipindi ambacho dunia, Tanzania ikiwemo inapitia katika changamoto mbalimbali za magonjwa kama vile Uviko 19 pamoja na magonjwa yasioambukiza. Aidha ameongeza kwamba serikali imedhamiria kufikisha huduma za kiafya katika maeneo yote hapa nchini na itaendelea kushirikiana na wadau wote wakiwemo watafiti na sekta binafsi.

Halikadhalika Makamu wa Rais ameiagiza Taasisi ya Taifa ya utafiti wa magonjwa ya binadamu (NIMR) kuongeza kasi ya ufanyaji utafiti pamoja na kuzalisha chanjo na dawa bora za asili.

Kwa upande wake Waziri wa Afya Ummy Mwalimu amesema wizara itaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa Taasisi ya Taifa ya utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) ili kuweza kutumiza majukumu yao kwa ufanisi. Amesema tayari NIMR imeshiriki katika tafiti mbalimbali zinazowezesha katika utungaji wa sera na mipango katika wizara ya afya ikiwemo kuwezesha Wizara kupata uhalisia wa utoaji wa chanjo ya HPV ambayo inakinga wasichana dhidi ya saratani ya mlango wa kizazi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...